Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 56 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 741 2023-06-27

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza:-

Je, nini kauli ya Serikali juu ya wafanyabiashara wa mazao ya misitu wanaozuiwa kufanya biashara na TFS?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Michael Costantino Mwakamo, Mbunge wa Kibaha Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Sheria ya Misitu Sura ya 323 na Kanuni zake za mwaka 2004 zimeelekeza utaratibu unaopaswa kufuatwa ili kuvuna, kusafirisha na kuuza mazao ya misitu kwa kuzingatia umiliki wa misitu au miti ambao ni ya watu binafsi, Serikali za vijiji, Serikali za mitaa au Serikali Kuu.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TFS haizuii kufanya biashara ya mazao ya misitu isipokuwa inasimamia sheria na kanuni ambazo zinahakikisha kunakuwa na usawa katika biashara hiyo pamoja na matumizi endelevu ya rasilimali za misitu nchini. Natoa rai kwa wadau au wafanyabiashara wote wenye nia njema ya kuvuna au kufanya biashara ya mazao ya misitu wafuate sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa ili kulinda misitu yetu ambayo ni muhimu sana kwa ustawi wa Taifa letu.