Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 56 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 743 2023-06-27

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza:-

Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya Lupingu hadi Kyela inayopita kandokando mwa Ziwa Nyasa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante na kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Zacharius Kamonga, Mbunge wa Ludewa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara ya Lupingu hadi Matema yenye urefu wa kilometa 126 ni barabara ya Mkoa na inahudumiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Njombe na Mkoa wa Mbeya na inapita sehemu zenye mvua nyingi, milima na miteremko mikali. Kwa upande wa Mkoa wa Njombe barabara hii inafunguliwa kwa awamu ambapo jumla ya kilometa 3.6 zimefunguliwa na kwa upande wa Mkoa wa Mbeya jumla ya kilometa 4.0 zimefunguliwa ikiwa ni pamoja na kufanya ujenzi wa daraja moja (box culvert) na drift moja. Serikali kupitia TANROADS itaendelea kuifungua barabara hii kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha, ahsante.