Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya Lupingu hadi Kyela inayopita kandokando mwa Ziwa Nyasa?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi na ningependa kuwa na maswali mawili madogo ya nyongeza.

Swali la kwanza; kwa kutambua umuhimu wa ulinzi na usalama wa mpaka ule wa Ziwa Nyasa na vivutio vya utalii, nini mkakati wa Serikali kuongeza fedha ili kasi ya ufunguaji wa barabara hii iongozeke?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; nini mpango wa Serikali kuongeza fedha kwenye barabara inayoanzia Mlangali – Lupila – Makete ili vikwazo vya eneo la Lusala na Ng’elamo viweze kuondolewa? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kwamba umuhimu wa barabara hii ukiachilia mbali kwamba ni barabara ya ulinzi, lakini pia wananchi wanaoishi kando kando ya ziwa hawana namna nyingine ya kuwasiliana panapokuwa kuna changamoto ya usafiri wa majini, ndiyo maana Serikali imeanza kwa awamu. Hata hivyo, mpango wa Serikali ni kutafuta fedha ambayo itaifungua hii barabara yote ambayo nimeielezea kwamba ni barabara ambayo inapita kwenye milima na mabonde makubwa sana. Kwa hiyo mpango huo upo ndiyo maana tumeanza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusu hii Barabara ya Mlangali kwenda Ikonda najua ni muhimu sana kuunganisha Ludewa na Makete na hasa Hospitali ya Ikonda. Serikali imetenga fedha mwaka huu kuhakikisha kwamba maeneo yote yale korofi inakarabatiwa ili iweze kupitika kwa kipindi chote, ahsante. (Makofi)