Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 56 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 744 2023-06-27

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Handeni – Kibirashi - Kondoa hadi Singida kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Reuben Nhamanilo Kwagilwa, Mbunge wa Handeni Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza ujenzi wa Barabara ya Handeni – Kibirashi – Kibaya – Chemba – Kwa Mtoro hadi Singida yenye urefu wa kilometa 424.24 kwa awamu. Ujenzi wa sehemu ya Handeni – Mafuleta kilometa 20 umefikia 11.61% na sehemu ya Mafuleta – Kileguru kilometa 30 mkataba umepelekwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa mapitio (vetting).

Mheshimiwa Spika, Kwa sehemu iliyobaki ya Kibirashi – Kwa Mtoro – Singida (km 384.33) utekelezaji wake upo kwenye miradi itakayojengwa kwa utaratibu wa Engineering, Procurement, Construction and Financing EPC+F). Hadi sasa Mkandarasi wa kujenga barabara hii amepatikana na mkataba wa kuanza ujenzi umesainiwa tarehe 16 Juni, 2023. Ahsante. (Makofi)