Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Handeni – Kibirashi - Kondoa hadi Singida kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa fursa hii ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; Kampuni hii ya Henan Highway Engineering Group iliyopewa kipande cha Handeni – Mafuleta kilometa 20, umepita mwaka mzima sasa tangu kampuni hii ipewe kandarasi hiyo, lakini ujenzi unasuasua. Kwa nini ujenzi huu unasuasua na unaenda kwa kuchelewa? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili la nyongeza; ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Turiani – Mziha – Handeni kilometa 104 kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Reuben Kwagilwa, Mbunge wa Handeni Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli mkandarasi hajaenda kwa speed ama kwa kasi ambayo tulikuwa tunaitegemea na hii ni kutokana na sababu kadhaa. Moja ya sababu wakati amekabidhiwa barabara hii kulikuwa na changamoto kubwa sana ya mahali pa kutolea materials ambayo ilichukua muda mrefu sana mpaka ku-acquire hilo eneo kwa sababu lilikuwa na mgogoro. Kwa sasa suala hilo limeshakamilishwa na sasa anaendelea kupata yale material ambayo alikuwa anahitaji kutoka kwenye hiyo sehemu ya kutolea materials.

Mheshimiwa Spika, suala lingine kulikuwa na changamoto kwenye management ya kwake, lakini hilo suala pia limeshakamilishwa. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kama alivyomsikia Waziri wa Fedha madai yale ya wakandarasi akiwepo huyu mkandarasi wa barabara hii ya Handeni – Mafuleta malipo yao yatatolewa ili waweze kuendelea, lakini pia wanapokuwa wanapewa kazi hawa wakandarasi moja ya sifa ni uwezo wao kifedha na hatutegemei akiwa 11% aweze kusimama, anatakiwa aendelee lakini pia vifaa ikiwa ni pamoja na management yake kwa kweli ndiyo maana wanafanyiwa due diligence. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na swali la pili, nataka nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba katika bajeti hii ambayo tunaendelea nayo tumetenga fedha kwa ajili ya kuanza ama kuendelea na ujenzi pale tulipoishia ya Turiani – Mziha hadi Handeni kwa mwaka ujao wa fedha, ahsante.