Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 56 Investment and Empowerment Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 746 2023-06-27

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:-

Je, lini mkataba na mwekezaji utakamilika ili Mradi wa Liganga na Mchuchuma uweze kufanya kazi na kuchangia pato la Taifa?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, nakushukuru, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Neema William Mgaya, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imedhamiria kuona mradi unganishi wa Liganga na Mchuchuma unatekelezwa, kwa kuzingatia dhamira hiyo, hatua mbalimbali zimeanza kuchukuliwa ili kuanza utekelezaji wa mradi huo muhimu. Hatua hizo ni pamoja na kulipa fidia ya kiasi cha shilingi za Kitanzania 15,424,364,900 kwa wananchi 1,142 na kuanza upya majadiliano na mwekezaji wa mradi ili kuhakikisha kuwa mradi unatekelezwa pasipo kuleta hasara kwa Taifa, nakushukuru. (Makofi)