Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 56 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 747 2023-06-27

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-

Je, lini Serikali itakamilisha usambazaji wa umeme wa REA katika Kata na Vijiji 23 vya Jimbo la Mbulu Vijijini?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati napenda kujibu swali la Mheshimiwa Flatei Gregory Massay, Mbunge wa Mbulu Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza mradi wa kusambaza umeme vijijini awamu ya tatu mzunguko wa II ambapo vijiji vyote visivyokuwa na umeme vitafikiwa na huduma ya umeme.

Mheshimiwa Spika, Mradi huu unahudumia vijiji 45 vilivyopo katika Jimbo la Mbulu Vijijini, ambapo kati ya hivyo, vjijiji 15 vimekwishawashiwa umeme na vijiji 30 kazi mbalimbali zinaendelea. Mradi huu unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Desemba, 2023. Nakushukuru.