Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha usambazaji wa umeme wa REA katika Kata na Vijiji 23 vya Jimbo la Mbulu Vijijini?

Supplementary Question 1

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Kata za Eshkesh, Yaeda Chini na wakati unajibu swali mwaka jana ulisema mwezi wa saba ndiyo watapata umeme lakini sasa umepeleka mwezi wa 12. Je, huoni kwamba utakuwa unatucheleweshea kupata umeme katika Kata hizi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili Waziri ametupa vijiji kadhaa ambavyo vitapa umeme kama underline. Kwa sisi wa vijijini, vijiji vyetu lazima umeme upelekwe ndio uweze kupatikana umeme na kama utapeleka umeme katika maeneo ya underline peke yake ni kwamba sisi wa vijijini hatutapata umeme.

Je, Mheshimiwa Waziri uko tayari sasa kubadilisha kauli hii na mpango huu ili kuhakikisha sisi wa vijijini tupate umeme?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Flatei Gregory Massay, Mbunge wa Mbulu Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli tulikuwa tunatarajia kumaliza mradi wa REA III Round II kwa awamu tofauti tofauti katika maeneo mbalimbali na sasa kwa walio wengi imekwenda mpaka Desemba mwaka huu na sababu kubwa ni mbili ambazo nyingine tulishazieleza huko nyuma za UVIKO na kuongezeka kwa bei za vifaa. Sababu nyingine iliongeza mwezi wa kumi wa mbili kuwa ndio deadline sasa ni kuongezeka kwa zile kilometa mbili ambapo Wakandarasi takribani wote 31 tayari wameshasaini ile mikataba ya kuongeza hilo loti kilometa mbili ili tuweze kuwa sasa kuwa na kilometa tatu za kupeleka umeme. Yote hiyo inatakiwa ikamilike kufikia mwezi Desemba.

Kwa hiyo, nimwombe Mheshimiwa Flatei pamoja na Waheshimiwa Wabunge wengine wote tusaidiane katika hili tumalize kazi hii ya upelekaji wa umeme katika vijiji vyote ifikapo Desemba mwaka huu ikiwa na extention ya hizo kilometa mbili.

Mheshimiwa Spika, kwenye swali la pili naamini alikuwa anazungumzia vitongozi japokuwa ametaja vijiji ambavyo viko underline, kwa sababu vijiji vyote vitakamilika Desenba mwaka huu. Tunafahamu kwamba tuna vitongoji 15 ambavyo tutapeleka kwa kila Jimbo. Kumekuwa kuna concern za Waheshimiwa Wabunge kwamba wapo ambao hawana vitongoji ambavyo viko chini ya line ambazo ni existing kwa sasa.

Mheshimiwa Spika, Serikali sikivu ya Daktari Samia Suluhu Hassan tumerudi tena mezani kutizama namna ambavyo tunaweza tukapanua wigo wa mradi na tunatafuta aidha tupate pesa ya nyongeza au tubadilishe procurement process ili tuweze kupata vifaa na kuwapa Wakandarasi kupeleka umeme kwenye vitongoji vyote.

Mheshimiwa Spika, hili tunalifanyia kazi na ninaamini litakuja na majibu mazuri katika muda mfupi ujao.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha usambazaji wa umeme wa REA katika Kata na Vijiji 23 vya Jimbo la Mbulu Vijijini?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Katika Mji wa Kasulu lipo tatizo la umeme kukatikakatika wakati wa mchana na kurudishwa usiku. Je, ni lini tatizo hilo litakwisha? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, katika maeneo yote ambayo kuna tatizo la kukatikakatika kwa umeme tunafatilia sababu huenda ni kuongezeka kwa mzigo au ni kutotosha kwa umeme tutafuatilia na hapo ili tatizo hilo tulimalize lakini tunaamini tukifikisha gridi kubwa Mkoa wa Kigoma tatizo hilo litakwisha kwa upana wake.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha usambazaji wa umeme wa REA katika Kata na Vijiji 23 vya Jimbo la Mbulu Vijijini?

Supplementary Question 3

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Katika Jimbo langu la Manyoni Magharibi vitongoji ambavyo viko underline havidi vitano.

Je, Serikali iko tayari sasa kutoa jibu la uhakika kwamba vitongoji katika Jimbo langu navyo vitapatiwa umeme?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye swali la msingi tunatafuta mbinu mbadala ambayo itatuwezesha kupata mradi utakaofikia vitongoji 15 vilivyo underline na visivyo underline kwenye Majimbo yote.

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha usambazaji wa umeme wa REA katika Kata na Vijiji 23 vya Jimbo la Mbulu Vijijini?

Supplementary Question 4

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Spika, ahsante katika vijiji vipya ambavyo mnapeleka umeme, kumekuwa na tatizo la Mkandarasi kufunga vifaa vilivyoko chini ya viwango na kusababisha umeme kukatikakatika na kukosa umeme zaidi ya siku 40.

Je, nini usimamizi wa Serikali kusababisha hili tatizo kutokuwepo?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, vifaa ambavyo tunavifunga kule tunavihakiki kabla ya kuvilipa, inawezekana labda ni matumizi vimefika muda wake lakini nimwombe Mheshimiwa Mbunge tutashirikiana kuhakikisha kwamba tunahakiki tatizo hasa ni nini kama ni vifaa mbavyo havikidhi basi tuviondoe na mkandarasi arekebishe tatizo hilo.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha usambazaji wa umeme wa REA katika Kata na Vijiji 23 vya Jimbo la Mbulu Vijijini?

Supplementary Question 5

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Mkandarasi anayeitwa Giza anasuasua sana miradi yake katika Jimbo la Kiteto. Je, ni lini miradi ya umeme ya vijiji vya Kiteto itakamilika?

SPIKA: Ni Mkandarasi wa umeme halafu anaitwa Giza?

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Spika, yes! Na miradi yake inasuasua.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, mkandarasi Giza Cables ni mkandarasi anayetoka Misri na Misri kuna Mji ambao unaitwa Giza na ndio jina lake linapotokea na alikuwa anafanya kazi Manyara na Mara. Ameshakamilisha loti yake ya Manyara na kwa Manyara tunaendelea kumsimamia ili akamilishe kazi yake kabla ya Desemba atakuwa amekamilisha kazi hiyo.

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha usambazaji wa umeme wa REA katika Kata na Vijiji 23 vya Jimbo la Mbulu Vijijini?

Supplementary Question 6

MHE. STELLA S. FIYAO: Mheshimiwa Spika, nashukuru ndani ya Halmashauri ya Mji wa Tunduma Kata ya Chiwezi bado haijafikiwa na umeme. Serikali mna mkakati gani wa kuhakikisha wananchi wa Chiwezi wanapata huduma ya umeme? Ahsante.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, wananchi wa Chiwezi watapata umeme kabla ya mwezi Desemba mwaka 2023.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha usambazaji wa umeme wa REA katika Kata na Vijiji 23 vya Jimbo la Mbulu Vijijini?

Supplementary Question 7

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, Serikali imefikia hatua gani kutafuta mkandarasi kwa ajili ya Visiwa vya Kilwa Kisiwani pamoja na Songo Mnara kupeleka umeme wa REA?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, wenzetu wa REA wanakamilisha mradi wa kupeleka umeme katika visiwa ambao unajitegema tofauti na wa REA kwa sababu REA inaunganisha kwenye gridi, lakini maeneo ya visiwani bado hatujaweza kufikisha gridi lakini tunakamilisha kwenye visiwa takribani kama 358 vya kupelekea umeme. Mradi huo utakapokamilika Mheshimiwa Kassinge ataona tukiutekeleza.

Name

Twaha Ally Mpembenwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha usambazaji wa umeme wa REA katika Kata na Vijiji 23 vya Jimbo la Mbulu Vijijini?

Supplementary Question 8

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE: Mheshimiwa Spika, nakushurukuru sana. Katikakatika ya umeme Jimbo la Kibiti, Rufiji, Mkuranga imekuwa ni donda sugu. Nini mkakati wa Serikali kukomesha tatizo hilo?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Pwani ni Mkoa wenye viwanda vingi sana na unao-consume umeme mwingi zaidi, lakini tunahakikisha kwamba katika mradi wetu wa Gridi Imara tunautizama kwa karibu ili kuhakikisha wanapata umeme wa kutosha na wa uhakika na katika eneo lake la Kibiti tatizo hilo litakwisha.