Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 55 Public Service Management Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 722 2023-06-26

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza: -

Je, utaratibu gani unatumika kutangaza ajira nchini ili kuhakikisha Watanzania wote wanapata haki ya kupata taarifa?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Ritta Enespher Kabati, swali namba 722, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Sera ya Menejimenti ya Ajira Toleo Na. 2 la mwaka 2008, Sura ya Nne, Aya ya 4(2) ikisomwa pamoja na ya Kanuni 12(1) ya Kanuni za Utumishi wa Umma za mwaka 2022, nafasi za ajira katika Utumishi wa Umma ni za ushindani na zinazingatia sifa, taaluma, uwazi na usawa.

Mheshimiwa Spika, kwa msingi huo, matangazo ya ajira kwa ajili ya kujaza nafasi wazi ndani ya Utumishi wa Umma hutolewa kupitia tovuti za taasisi husika, mitandao ya jamii, magazeti na mbao za matangazo katika ofisi husika. Maombi ya nafasi hizi hudumu kwa muda wa siku kumi na nne 14 kwa kada za masharti ya kawaida na siku 21 kwa waombaji wa nafasi za Watendaji Wakuu na nafasi za Uongozi za Taasisi za Kimkakati.