Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza: - Je, utaratibu gani unatumika kutangaza ajira nchini ili kuhakikisha Watanzania wote wanapata haki ya kupata taarifa?

Supplementary Question 1

MHE DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza.

Ni kwa nini sasa Serikali inapoita vijana kwa ajili ya usaili isiangalie hizo sifa na vigezo kuliko hivi sasa pengine nafasi ni ishirini wanaitwa watoto 3,000 mpaka 5,000? Wanasababisha vijana wengi kuteseka hapa Dodoma wakati wa kusubiri huo usaili. (Makofi)

Swali langu la pili, ni kwa nini vijana wengi wamekuwa wakijitolea au kupewa nafasi za mikataba lakini inapotokea ajira hawa vijana hawapati kipaumbele, wamekuwa wakijitolea miaka minne, mitano kiasi kwamba zikitoka ajira wanaajiriwa wapya. Hii kwa kweli inaumiza sana na inaliza sana kwa vijana wetu. (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali maswali mawili ya Mheshimiwa Ritta Kabati kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na nafasi chache wanaitwa wengi, katika maelezo ya msingi nilieleza kwamba nafasi za ajira kwa sasa kwa mujibu wa kanuni ambazo zimepitishwa na Bunge lako ni nafasi za kiushindani. Hivyo tunapotangaza matangazo matarajio yetu ni kwamba watajitokeza wengi ili waje kushindana kwa ajili ya kupata nafasi hizo.

Mheshimiwa Spika, ni kweli nakiri mbele ya Bunge lako kwamba malalamiko juu ya wingi wa wanaoomba na dhidi ya nafasi kuwa chache umeendelea kujitokeza. Serikali yako imeendelea kufanya juhudi za dhati kuhakikisha kwamba tunakabiliana na changamoto hii. Lakini kupitia Bunge lako maelekezo yalishatolewa na Ofisi ya Rais inayoshughulikia Utumishi imeyachukua na inakwenda kuyafanyia kazi na tutapokuwa tayari tutaleta majibu mbele ya Bunge lako.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili kuhusu wale wanaojitolea halafu baadaye wanakuja kukosa ajira. Wakati naeleza katika swali la msingi, ajira za Serikali zinazingatia sifa, taaluma, uwazi na usawa, na ni maelekezo ya Bunge lako kwamba katika uwazi huo na usawa huo, ulielekeza kwamba ajira zinapotolewa waitwe watu wadahiliwe kwa usawa na uwazi, sasa inapotokea kwamba mtu aliyepo kazini anakosa kazi hili tena linakuwa niseme ni jambo la kiufundi zaidi na siyo jambo la mtu kuonewa. Kwa hiyo, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba wanaofanya kazi waendelee kuhakikisha kwamba wanashindana vizuri ili waendelee kupata kazi kama ambavyo wengine wamekuja kwenye ushindani.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza: - Je, utaratibu gani unatumika kutangaza ajira nchini ili kuhakikisha Watanzania wote wanapata haki ya kupata taarifa?

Supplementary Question 2

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa kuwa Waziri ametamka wazi kwamba nafasi hizi zinatolewa kwa ushindani, lakini kule vijijini ambako wanafunzi wengi ambao wanaomba hizi nafasi ndiko waliko, Magazeti hayafiki wala mtandao hakuna.

Je, huo ushindani wa haki unapatikanaje katika mazingira ya aina hiyo? (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Shangazi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba, vilio vinekuwepo hasa katika maeneo ya kule vijijini kabisa, na ni maelekezo yetu kama Wizara kuhakikisha kwamba matangazo yote yanayoletwa ya ajira yanakwenda kwa Wakurugenzi wote wa Halmashauri na kuhakikisha yanafika kwenye vijiji husika, yafike kwenye ofisi za vijiji, yafike kwenye ofisi za kata na maeneo yote yaliyo muhimu kwa ajili ya wananchi kupata taarifa, ili ajira hizi ziendelee kukimbiliwa na Watanzania wote kwa usawa.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza: - Je, utaratibu gani unatumika kutangaza ajira nchini ili kuhakikisha Watanzania wote wanapata haki ya kupata taarifa?

Supplementary Question 3

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa jambo la kuita watu wengi kwenye nafasi chache chache za usaili limekuwa ni jambo sugu na Serikali hamuwezi kulifanyia kazi; je, hamuoni sasa umefika wakati kuwapa posho angalau wale mnaowaita, ili waweze kujikimu wanapokuwa Dodoma?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zuberi Kuchauka kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, jambo analosema la kutoa posho kwa wanaoomba, hili ni jambo la kibajeti, lakini pia ni jambo la kisera. Kwa hiyo, tutakapokuwa tumejenga uwezo, Mheshimiwa Zuberi Kuchauka na Wabunge wote basi nalo pia litaangaliwa, lakini kwa sasa niseme jambo hilo ni gumu kidogo. (Makofi)

Name

Janejelly Ntate James

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza: - Je, utaratibu gani unatumika kutangaza ajira nchini ili kuhakikisha Watanzania wote wanapata haki ya kupata taarifa?

Supplementary Question 4

MHE. JANEJELLY J. NTATE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, tunajua wanaotakiwa kuajiri Serikali Kuu ni Menejimenti hya Utumishi kupitia Sekretarieti ya Ajira; je, ni lini Serikali sasa itachukua hilo jukumu badala ya kuachia idara zinazojitegemea? Kuachia Wizara nyingine kuajiri watumishi wa Serikali?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Janejelly Ntate kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli Serikali iliamua kugatua baadhi ya mamlaka yake na kupeleka kwenye Taasisi na Wizara mbalimbali ili kupunguza lile lundo la watu wote kuja katika sehemu moja, lakini pia tukizingatia professional katika uajiri, lakini mawazo anayotoa Mheshimiwa Mbunge ni mawazo ambayo hata sisi ndani ya Wizara tunayaangalia, lakini nataka nikuhakikishie kwamba mambo yote haya yanakwenda kisera, kimkakati, na baada ya kujiridhisha kwamba tutakapoyachukua kuyarudisha Wizarani au kuendelea kufanya katika njia nyingine yatakuwa na tija kwa ajili ya kusaidia Watanzania inapofika kwenye jambo zima la ajira.

Mheshimiwa Spika, nataka nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge, mawazo yako ni mazuri, na sisi kama Wizara tuyachukue na kuendelea kuyafanyia kazi na tutakuja kujulishana vizuri baadae. (Makofi)

Name

Amandus Julius Chinguile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza: - Je, utaratibu gani unatumika kutangaza ajira nchini ili kuhakikisha Watanzania wote wanapata haki ya kupata taarifa?

Supplementary Question 5

MHE. AMANDUS J. CHINGUILE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mfumo wa ajira ulioko sasa una manung’uniko mengi; Serikali haioni iko haja sasa ya kupitia mfumo wenyewe kwa ujumla ili uwe rafiki kwa vijana wetu walioko? (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Amandus kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, wakati tunawasilisha bajeti ya Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, hoja anayoeleza Mheshimiwa Mbunge ilitolewa pia katika kikao kile na yalikuwa ni makubaliano ya Bunge lako kwamba tutayachukua mawazo mazuri yale na kwenda kuyafanyia kazi, na haya yote yatakapokuwa yamekamilika basi yatakuja kuonekana katika sera na sheria ambazo baadae nafikiri zinaweza zikabadilika kutokana na mawazo mazuri ya Bunge lako.

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba maagizo ya Bunge yanaendelea kufanyiwa kazi, na tutakapokuwa tayari tutakuja kuleta taarifa katika utaratibu wa vile vikao vyetu.