Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 54 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 706 2023-06-23

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza:-

Je, ni lini Barabara kutoka Kijiji cha Kalenga kupitia Kata za Ulanda, Maboga, Wasa - Madibila zitapandishwa kuwa za Mkoa?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jackson Gedion Kiswaga, Mbunge wa Jimbo la Kalenga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Barabara Namba 13 ya Mwaka 2007, kifungu cha 11 na Kanuni za Usimamizi wa Barabara ya Mwaka 2009, Kifungu cha 43(1) na (2) na kifungu cha 44(1) kupitia Tangazo la Serikali Namba 21 la tarehe 23 Januari, 2009, limeainisha vigezo vya utaratibu wa kupandisha au kuteremsha hadhi barabara toka daraja moja kwenda daraja lingine.

Mheshimiwa Spika, mapitio ya upandishaji hadhi wa barabara hii ulifanyika mwaka 2019 na Wizara Ujenzi na Uchukuzi, yalibaini barabara hiyo kukosa sifa kama barabara ya mkoa (regional road) na hivyo kupewa hadhi ya barabara za Wilaya katika kundi la mkusanyo (collector roads).