Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza:- Je, ni lini Barabara kutoka Kijiji cha Kalenga kupitia Kata za Ulanda, Maboga, Wasa - Madibila zitapandishwa kuwa za Mkoa?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize maswali madogo mawili ya nyongeza. Kwa kuwa Barabara ya Kalenga – Wasa - Mafinga ni barabara muhimu sana kwa uchumi katika Mkoa wetu wa Iringa. Je, katika kilometa 100 za Mradi wa RISE kwa nini wasipatiwe japo kilometa 10 tu? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; Barabara ya Itimbo – Kitelewasi inapita katika milima na miteremko mikali, hivyo inahitaji kujengewa makalavati. Je, Serikali ipo tayari sasa kujenga makalavati ili wananchi wa Kitelewasi na Itimbo waweze kupita kwa uraisi? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Sika, ahsante sana. Kwanza natambua kwamba kuna mahitaji makubwa ya ujenzi wa barabara hususani katika maeneo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameainisha. Barabara ya Kalenga mpaka Mafinga ambayo ina urefu wa kilometa 100 hususani hizi za RISE na amekuwa akiomba kilometa kumi, niseme tu kwamba zile barabara zimeshawekwa katika mpango wake. Kwa hiyo kikubwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI itazingatia katika mipango ijayo ili kuona sasa tunatafuta hizo kilometa 10 waweze kujenga katika maeneo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyataja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusu Barabara ya Itimbo – Kitelewasi ambayo ina mteremko mkali, mahitaji ya Kalavati, nafikiri kwa kutumia fedha za Mfuko wa Dharura, Ofisi ya TARURA Mkoa wa Iringa tuwaelekeze tu kwamba kulingana na mahitaji ya maeneo hayo, waipe kipaumbele barabara hii, ahsante sana. (Makofi)