Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 54 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 707 2023-06-23

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU K.n.y. MHE. IDDI K. IDDI aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itajenga mitaro ya kuchepushia maji katika Kata za Bulyanhulu, Segese, Ngaya na Bulige?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Idd Kassim Idd, Mbunge wa Msalala, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Kata za Bulyanhulu na Segese zinapitiwa na Barabara ya Kahama hadi Kakola ambayo ipo kwenye mpango wa kuanza kujengwa kwa kiwango cha lami katika mwaka wa fedha 2023/2024. Taratibu za manunuzi kwa ajili ya ujenzi zinaendelea na ujenzi wa mitaro utafanyika wakati wa utekelezaji wa mradi huo. Aidha, Mji Mdogo wa Bulige unapitiwa na Barabara ya Kahama – Solwa ambapo ujenzi kwa kiwango cha lami unaendelea na utahusisha ujenzi wa mitaro. Vilevile, mitaro iliyopo katika Kata ya Ngaya inakidhi mahitaji ya barabara hiyo na itaendelea kufanyiwa matengenezo, ahsante.