Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU K.n.y. MHE. IDDI K. IDDI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga mitaro ya kuchepushia maji katika Kata za Bulyanhulu, Segese, Ngaya na Bulige?

Supplementary Question 1

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu ya Serikali, lakini naomba niulize swali moja la nyongeza. Kwa sababu suala la ujenzi wa barabara tunatumia fedha nyingi na maeneo mengine mvua zimekuwa zikiharibu miundombinu hii, hii ni kwa sababu labda hatukufanya design au hatukufanya utafiti wa kutosha kwenye athari ya kimazingira. Je, ni nini mkakati wa Serikali katika kuhakikisha kwamba kabla ya ujenzi wa miundombinu hii ambayo inatumia gharama kubwa kuangalia athari za kimazingira zisilete matatizo katika miundombinu? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge Mtaturu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba barabara na hasa hizi za udongo na za changalawe mara nyingi zinaharibika hasa kipindi cha mvua na Serikali imekuwa ikitenga fedha nyingi kwa ajili ya kufanya ukarabati na hasa kutengeneza mitaro na mifereji ili kutoa hayo maji, kwa sababu moja ya chanzo kikubwa cha kuharibu barabara ni maji. Pia Serikali inaendelea kutoa elimu kwa wananchi kutotumia barabara kwenye hifadhi za barabara na kupitisha mifugo kwenye barabara. Kwa sababu hicho pia ndiyo chanzo kikubwa cha kufanya uharibifu wa barabara, kwa sababu ukishalima karibu na barabara unatuamisha maji na hivyo barabara zinaharibika. Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU K.n.y. MHE. IDDI K. IDDI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga mitaro ya kuchepushia maji katika Kata za Bulyanhulu, Segese, Ngaya na Bulige?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Barabara ya Kagoma – Biharamulo katika Mji wa Muleba pale, walielekeza maji kwenye makazi yatu ambapo wamechimba mtaro mkubwa ambao unajulikana kama Buhimba, lakini Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano wakati wa Kampeni 2020 - 2025 alitoa maelekezo mahususi kwamba Mamlaka zinazohusika wakae tumalize hilo tatizo: -

Je ni lini Mamlaka ya TANROADS itakuja kumaliza tatizo la maji katika eneo la Buhimba? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa sababu yalikuwa ni maelekezo mahususi na kuhusu eneo mahususi, naomba pia kutumia nafasi hii kumwelekeza Meneja wa Mkoa wa Kagera aende kwenye eneo lililokuwa limetolewa maelekezo na Mheshimiwa Rais, kutoa ama kuyatoa maji yaliyokuwa yameelekezwa kwenye makazi ya watu na kuyapitisha kwenye njia sahihi. Nimwombe atakapokuwa anafanya hivyo aweze kuwasiliana na Mheshimiwa Mbunge ambaye ametoa hoja hii, ahsante. (Makofi)