Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 54 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 708 2023-06-23

Name

Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza:-

Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Mpanda hadi Uvinza, yenye kilometa 159, utakamilika?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Taska Restituta Mbogo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza ujenzi kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Mpanda hadi Uvinza yenye urefu wa kilometa 194 kwa awamu. Ujenzi wa Barabara ya Mpanda hadi Vikonge kilometa 37.6 umekamilika na ujenzi wa sehemu ya Vikonge hadi Luhafwe kilometa 25 unaendelea. Mkataba wa ujenzi wa sehemu ya Luhafwe hadi Mishamo unatarajiwa kusainiwa kabla ya mwisho wa mwezi Juni, 2023. Kwa sehemu iliyobaki ya Mishamo – Uvinza kilometa 94, Serikali iko kwenye mazungumzo na Benki ya Maendeleo ya Afrika ili kuruhusu bakaa ya fedha za Mradi wa Ujenzi wa Barabara ya Tabora – Koga hadi Mpanda zitumike katika ujenzi wa sehemu hii, ahsante.