Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Mpanda hadi Uvinza, yenye kilometa 159, utakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. TASKA R. MBOGO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali ninayo maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha inatuongezea pesa na wakandarasi zaidi ya mmoja, wawe watatu ili Barabara ya Mpanda – Kigoma ikamilike ili wananchi wa Mkoa wa Katavi waweze kufunguka? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; je, mazungumzo hayo na Benki ya Afrika yatakamilika lini? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika taratibu za kandarasi inategemea na mlivyopanga lots ama vipande na vipande tunavyovijenga hakuna ambacho kwa sasa kinazidi kilometa 50.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo katika hivyo vipande vitatu vinavyojengwa kila kipande kina mkandarasi lakini tunategemea katika swali lake la pili kama African Development Bank tutakuwa tumekubaliana nao kutumia bakaa iliyobaki kukamilisha hiyo barabara kwa urefu wa kilometa 94 ni wazi kwamba hatutakuwa na mkandarasi mmoja tutakuwa na zaidi ya mkandarasi mmoja ili kukamilisha kazi kwa haraka kati ya Mpanda na Uvinza kwa kilometa 94 ambazo zimebaki, ahsante.