Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 54 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 714 2023-06-23

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza:-

Je, lini Serikali italeta Bungeni Muswada wa Sheria wa kulinda ardhi ya Kilimo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Naghenjwa Livingstone Kaboyoka, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kulinda ardhi ya kilimo kama ilivyobainishwa katika Sera ya Taifa ya Kilimo ya mwaka 2013. Kwa msingi huo, Wizara inapitia na kuchambua Sheria Mbalimbali zinazohusiana na usimamizi na matumizi ya ardhi ya kilimo ikiwemo Sheria ya Ardhi ya Vijiji, Sura ya 114, Sheria ya Ardhi, Sura ya 113 na Sheria ya Mipango ya Matumizi bora ya Ardhi, Sura ya 116 na Sheria ya Utwaaji wa Ardhi, Sura ya 118.

Mheshimiwa Spika, uchambuzi huo utabainisha upungufu uliopo katika sheria hizo na kuainisha maeneo ambayo yatajumuishwa kwenye Sheria ya Maendeleo ya Kilimo inayopendekezwa kutugwa ambayo itakuwa na sehemu ya masuala ya usimamizi wa ardhi ya kilimo. Baada ya uchambuzi huo wa kitaalam, itawasilishwa kwenye ngazi za maamuzi kuhusu mapendekezo ya sheria hiyo.