Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza:- Je, lini Serikali italeta Bungeni Muswada wa Sheria wa kulinda ardhi ya Kilimo?

Supplementary Question 1

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri, nataka kumkumbusha tu kwamba, pamoja na kwamba nchi yetu kuwa na ukubwa wa eneo lenye square kilometer 947,300 eneo linalofaa kwa kilimo ni hekta milioni 44 tu.

Je, Serikali haioni wakati umefika kuharakisha kutunga sheria itakayolinda eneo hili la kilimo ili lisije likavamiwa kwa shughuli nyingine? Ahsante. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kumjibu Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kuilinda ardhi kwa ajili ya kilimo. Kama nilivyosema hapa, tumeamua kupitia baadhi ya sheria ili mwisho wa siku tuje na sheria ambayo imekamilika. Nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaharakisha mchakato huu ili mwisho wa siku tupate sheria yetu ya kilimo, tutunze ardhi ya kilimo.

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwanza namshukuru Naibu Waziri wa Kilimo kwa majibu yake mazuri aliyoyajibu kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, lakini nilichotaka kusema tu ni kwamba, Wizara ya Ardhi pamoja na Wizara ya Kilimo tumeshaanza mchakato wa kuyatambua yale maeneo ambayo yanafaa kwa kilimo. Kwa hatua ya kwanza itakayofanyika ni kuya-gazette ili yasiweze kuingiliwa na watu wengine. Kwa hiyo, stage nyingine itakayofuata ndiyo hiyo ya kutunga sheria ili kuyalinda kwa ajili ya uhifadhi wa kilimo. (Makofi)