Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 54 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 715 2023-06-23

Name

Anton Albert Mwantona

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza:-

Je, lini Serikali itapeleka Umeme wa REA katika vijiji na vitongoji ambavyo vimeshawekewa nguzo Jimbo la Rungwe?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anton Albert Mwantona, Mbunge wa Rungwe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika Wilaya ya Rungwe, mkandarasi M/S State Grid Ltd. anakamilisha maandalizi ya vifaa vya ujenzi wa maeneo yaliyobaki na kazi zinatarajiwa kuanza tarehe 1 Julai, 2023 na kukamilika mwezi Oktoba, 2023. Pamoja na miradi mingine katika bajeti ya mwaka 2023/2024, kila Jimbo limetengewa bajeti ya kupelekewa umeme katika vitongoji 15 vya kuanzia wakati maandalizi ya mradi wa Hamlet Electrification Project (HEP) unaotarajiwa kuanza mwaka 2024/2025 yanakamilika, nakushukuru.