Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anton Albert Mwantona

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka Umeme wa REA katika vijiji na vitongoji ambavyo vimeshawekewa nguzo Jimbo la Rungwe?

Supplementary Question 1

MHE. ANTON A. MWANTONA: Mheshimiwa Spika, kwanza napenda nipate ufafanuzi zaidi kwenye jibu la msingi. Mkandarasi anayetekeleza mradi sasa hivi kule Rungwe ni ETDCO siyo State Grid Limited. Kwa hiyo, nilikuwa naomba nipate ufafanuzi zaidi kwamba, huyu State Grid Limited ameingiaje hapo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Kwenye REA II kuna vijiji 25 viliachwa, vilitelekezwa, yaani kama viporo; napenda nijue kwamba ni lini huu Mradi wa REA II vijiji 25 utaanza kutekelezwa? Ahsante. (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Mkandarasi ETDCO ndio yuko site na Mkandarasi ETDCO anatekeleza Mradi wa REA III Round II. Ndiyo mradi unaoendelea ambao ni mkubwa ambao ETDCO anautekeleza na tunatarajia itakapofika Desemba atakuwa amemaliza kwa sababu, ni katika ile azma ya kuhakikisha vijiji vyote vinapata umeme ifikapo Desemba.

Mheshimiwa Spika, kwenye swali la pili sasa lililosema la vijiji 25 ambavyo vilikuwa vimeachwa na REA Awamu ya Pili tulikuwa tuna mabishano na mkandarasi kuhusu wigo wa utekelezaji na namna ya utekelezaji. Kuna maeneo alisimamisha nguzo, kuna maeneo aliweka waya halafu akaondoka, baada ya mvutano wa muda mrefu, ndiyo sasa tumemrudisha yeye mwenyewe, huyu huyu State Grid, ili aje kukamilisha vile vijiji vyake 25 ambavyo alikuwa ameviacha. Ndiyo maana tunasema ataanza Julai na atamaliza mwezi wa Kumi wakati ETDCO alianza tangu mwaka juzi, atamaliza Desemba mwaka huu.

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka Umeme wa REA katika vijiji na vitongoji ambavyo vimeshawekewa nguzo Jimbo la Rungwe?

Supplementary Question 2

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Je, ni lini Serikali itapeleka umeme kwenye vijiji vya Kata ya Shizuvi ambavyo ni sehemu ya REA Awamu ya Tatu, Mzunguko wa Pili?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, vijiji vyote ambavyo viko kwenye Mradi wa REA Awamu ya Tatu, Mzunguko wa Pili, vitakamilika ifikapo Desemba mwaka huu wa 2023. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Oran Manase Njeza kwamba vijiji hivyo pia katika kata hizo vitakuwa vimefikiwa na umeme kabla ya Desemba mwaka huu 2023.

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka Umeme wa REA katika vijiji na vitongoji ambavyo vimeshawekewa nguzo Jimbo la Rungwe?

Supplementary Question 3

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Katika vijiji 15 alivyovitaja vya vitongoji kumekuwa na changamoto kidogo kwa sababu, tulishapeleka vijiji 15 wakasema kwamba vijiji hivyo havitambuliki na TAMISEMI, lakini pia wakatoa condition nyingine kwamba vijiji hivyo lazima vipitiwe na mkondo mkuu wa waya.

Je, Serikali inatoa maelezo gani ya msingi kwa sababu inaonekana kule wale watendaji hawana uhakika wa kitu gani cha kutekeleza? (Makofi)

SPIKA: Nilikuwa najaribu kusikiliza kama swali lako linahusiana na swali la msingi au Hapana? Maana umetoa maelezo ya ziada hapo mwanzo yanayokuondoa kwenye swali la msingi. Swali lako ni nini? Uliza swali bila maelezo, itakusaidia kuwa kwenye swali la msingi

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Spika, vitongoji 15 alivyovitaja kwamba ndiyo vinatakiwa vipitiwe kwa ¬level hii ya umeme aliyoisema sasa hivi kunakuwa na mkanganyiko, wale watekelezaji hawajui kwamba watekeleze vipi? Kwa sababu, ukiwapelekea vitongoji wanasema ah, ah, vitongoji hivi havistahili kwa sababu, hakuna umeme. Sasa je, kuna condition ya vitongoji au hakuna condition kwamba, vitongoji vyovyote vinaweza kuwekewa au kuna condition fulani lazima ndiyo vipelekewe huo umeme?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, katika vitongoji 15 ambavyo tumepata fedha ya kuvipelekea umeme katika mradi huu utakaotekelezwa mwaka 2023/2024 nieleze wazi kwamba ni vitongiji ambavyo tunaviita underline. Ni vitongoji ambavyo tayari miundombinu ya umeme mkubwa ilishapita katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, unakuta kwenye kijiji kimoja chenye vitongoji labda vitano, vitongoji viwili vimefikiwa na miundombinu kwa maana ya kuwashwa, kitongoji kimoja miundombinu imepita kwa juu haijashuka kwenye kile kitongoji na labda vitongoji vingine viwili havijafikiwa kabisa na umeme mkubwa na havijafikiwa na umeme mdogo.

Mheshimiwa Spika, fedha hii ndogo tuliyoipata Shilingi bilioni 379 inatosha kwa kupeleka miundombinu ya umeme mdogo tu katika yale maeneo ambayo tayari miundombinu ya umeme mkubwa ilishapita. Kwa hiyo, wale watendaji wenzetu kule chini wanayo maelekezo haya na wanajua namna ya kuwasilisha maelezo haya. Wataleta vile vitongoji ambavyo vilishapitiwa na line kubwa, sasa tunashusha umeme kwa ajili ya kujazia katika maeneo hayo. Pia mwaka 2024/2025 kwenye mradi wetu mkubwa wa HEP wa shilingi trilioni sita hapo tutakwenda kumaliza vitongoji vyote ambavyo vilishafikiwa na ambavyo havijafikiwa na miundombinu ya umeme.

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka Umeme wa REA katika vijiji na vitongoji ambavyo vimeshawekewa nguzo Jimbo la Rungwe?

Supplementary Question 4

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii. Katika Kata ya Tarada, Kijiji cha Ngunga upo mradi wa nguvu za jua ambao ni wa gharama ya shilingi bilioni 275. Zoezi la kulipa fidia kwa waathirika bado limeanza kusuasua kutokana na changamoto ya migogoro ya maeneo.

Je, Waziri yuko tayari kufika katika eneo hilo ilimradi kutatua kwa haraka tatizo hilo na mradi huu uanze kutekelezwa kwa haraka? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa ameuliza kama Mheshimiwa Waziri yuko tayari kufika katika eneo hilo, ninayo hakika kwamba dhati ya moyo wake, lakini na sisi wasaidizi wake Wizarani tutafika na kuweza kuona tatizo ni nini kwa kushirikiana na wenzetu wa Wizara ya Ardhi ili tuweze kulitatua. Kwa kuonesha nia ya dhati, tayari na mkataba wa utekelezaji wa mradi ule umeshasainiwa. Hivyo, hizi changamoto nyingine ambazo zitazuia utekelezaji hatuwezi kukubaliana nazo. Tutafika ili tutatue tatizo na mradi uanze mara moja.