Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 54 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 716 2023-06-23

Name

Ng'wasi Damas Kamani

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NG’WASI D. KAMANI aliuliza:-

Je, nini mkakati wa kuongeza nguvu kwenye uvuvi ili vijana wa Mkoa wa Mwanza na Kanda ya Ziwa wanufaike na Ziwa Victoria?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ng’wasi Damas Kamani, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imetenga fedha kwa ajili ya kuwawezesha wavuvi boti za kisasa kwa mkopo usio na riba kupitia Benki ya Kilimo Tanzania (TADB). Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na TADB inakamilisha taratibu za kutoa maboti 158 kwa mkopo kwa Vyama vya Ushirika 45, Vikundi vya Wavuvi 71 na watu binafsi 43 ambao wengi wao ni vijana. Aidha, katika Ukanda wa Ziwa Victoria, jumla ya Vyama vya Ushirika 20 kwa maana ya Mkoa wa Mwanza 14, Vikundi 17 kwa maana ya Mkoa wa Mwanza 10, na watu binafsi 17 kwa Mwanza wanne, wanatarajiwa kunufaika na mkopo wa maboti hayo.

Mheshimiwa Spika, vilevile Serikali imetenga fedha kwa ajili ya miradi ya ufugaji samaki kwenye vizimba katika Ziwa Victoria kwa kuwawezesha vijana kupata pembejeo za ufugaji samaki kwa mikopo isiyo na riba. Aidha, jumla ya wanufaika 3,154 ambao wengi wao ni vijana wameainishwa kunufaika na mkopo huo ikijumuisha vikundi 67, kwa maana ya Mwanza 42, vyama vya ushirika 24, Mwanza 14; kampuni 10, kwa Mkoa wa Mwanza vitano; na watu binafsi 32, kwa Mkoa wa Mwanza 16 kutoka ukanda wa Ziwa Victoria.