Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ng'wasi Damas Kamani

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NG’WASI D. KAMANI aliuliza:- Je, nini mkakati wa kuongeza nguvu kwenye uvuvi ili vijana wa Mkoa wa Mwanza na Kanda ya Ziwa wanufaike na Ziwa Victoria?

Supplementary Question 1

MHE. NG’WASI D. KAMANI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kuona potential iliyoko kwenye Ziwa Viktoria na haja ya kulitumia ziwa hili kuweza kutatua changamoto za kiuchumi na ajira kwa vijana walioko katika Kanda ya Ziwa na Tanzania kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, nina maswali mawili ya nyongeza. Kwanza fedha hizi zimetengwa takribani Shilingi bilioni 20 kwa mwaka wa fedha 2022/2023; na tunavyozungumza sasa utaratibu ulianza tangu mwaka 2022 na sasa tumebakiwa na kama siku saba tu kumaliza mwaka huu wa fedha 2022/2023; naomba commitment ya Serikali: Ni lini hasa utekelezaji wa mradi huu utaanza kwa sababu, taratibu zote za awali zimeshatimia?

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Kwa vile tayari kuna sintofahamu na changamoto fulani kwa vijana wa Mwanza na Mikoa yote ambayo inahusika na mradi huu ambazo baadhi yake nilizungumza jana: Je, Serikali au Waziri na wasaidizi wake wako tayari kuambatana nami baada ya Bunge hili la Bajeti kwenda kuwasikiliza vijana wanaonufaika na mradi huu juu ya changamoto na sintofahamu zao kuweza kuzitatua? Ahsante. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia jambo hili kwa ukaribu kabisa. Nimhakikishie tu kwamba tuko katika hatua za mwisho za maandalizi za ugawaji wa hivi vifaa, hususan maboti kwa wavuvi wa Kanda ya Ziwa Victoria. Uzinduzi huu tutafanyia huko huko ukanda wa Ziwa Viktoria. Kwa hiyo, tuko katika hatua za mwisho na ninaamini ndani ya muda mfupi Wizara ya Mifugo na Uvuvi itataja hiyo tarehe rasmi ya lini sasa tunatoa vifaa hivyo.

Mheshimiwa Spika, kuhusu kuambatana na Mheshimiwa Mbunge, mimi pamoja na Mheshimiwa Waziri tuko tayari muda wowote mara baada ya Bunge lako kuahirishwa, ahsante sana. (Makofi)