Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 53 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 699 2023-06-22

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. FURAHA N. MATONDO K.n.y. MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: -

Je, lini kipande cha barabara cha Kisorya hadi Nansio kitaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Michael Mkundi, Mbunge wa Ukerewe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inajenga barabara ya Nyamuswa – Bunda – Kisorya – Nansio yenye urefu wa kilometa 121.9 kwa awamu. Ujenzi kwa kiwango cha lami awamu ya kwanza sehemu ya Bulamba – Kisorya kilometa 51 umekamilika. Kwa sehemu ya Nyamuswa – Bunda – Bulamba kilometa 56.4 ujenzi umekamilika na upo kwenye kipindi cha matazamio huku Mkandarasi akimalizia kazi ndogo ndogo zilizobaki. Kwa sehemu iliyobaki ya kutoka Kisorya hadi Nansio ambayo ina urefu wa kilometa 12.8 Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi. Ahsante.