Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FURAHA N. MATONDO K.n.y. MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: - Je, lini kipande cha barabara cha Kisorya hadi Nansio kitaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. FURAHA M. MATONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Ukerewe ni kisiwa na kwenye bajeti ya mwaka huu Serikali imetenga fedha ya kujenga barabara hiyo ya kutoka Kisorya kwenda Nansio. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi huo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Furaha Matondo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli dhamira ya Serikali ni kuijenga barabara yote kwa kiwango cha lami na Mheshimiwa Mbunge atakubaliana na mimi kwamba tayari tumeshajenga sehemu kubwa ya hiyo barabara. Hela iliyotengwa ilikuwa kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa daraja ambalo lina kilometa takribani moja, lakini kwa maombi ya wana Ukerewe na Mheshimiwa Mbunge wa Ukerewe, wameomba badala ya kuanza daraja kwa kuwa tunavyo vivuko viwili vikubwa ambavyo vitaendela kufanya kazi na hasa baada ya kuongeza kivuko kipya ni bora tukajenga barabara ya lami kuanzia Lugenzi hadi Nansio na wakati Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi anawasilisha bajeti alitoa commitment kwamba tutaanza kujenga mwaka ujao wa fedha barabara hii kwa kiwango cha lami kuanzia Nansio kuja Lugezi. Ahsante.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. FURAHA N. MATONDO K.n.y. MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: - Je, lini kipande cha barabara cha Kisorya hadi Nansio kitaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi. Wakati wa ziara ya Mheshimiwa Rais mwaka jana iliahidiwa kujengwa barabara kutoka Mafinga inayokwenda Madibila kupitia Sadani.

Je, ni lini ujenzi wa barabara hiyo utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cosato Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli swali hili limeulizwa jana na Mheshimiwa nakumbuka wa Mbarali na nilijibu kwamba tutaendelea kulitengeneza, lakini marekebisho tu ni kwamba, kama alivyosema wakati Mheshimiwa Rais ametembelea Mkoa wa Iringa, Wabunge wa Mkoa wa Iringa hasa Wilaya ya Mufindi waliomba barabara hiyo ijengwe kwa kiwango cha lami na Mheshimiwa Rais alitoa ahadi na akatoa maelekezo na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi akiwepo, ameshatoa maelekezo, kwamba ile ahadi ya Rais ianze kutekelezwa mwaka huu. Kwa hiyo, tutaanza kuijenga hiyo barabara kwa kiwango cha lami kama maagizo ya Mheshimiwa Rais yalivyotolewa kuanzia huku Mafinga kwenda Mbarali, ahsante. (Makofi)

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. FURAHA N. MATONDO K.n.y. MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: - Je, lini kipande cha barabara cha Kisorya hadi Nansio kitaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa hii nafasi. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami kipande cha barabara kinachoanzia Ngarenanyuki hadi Oldonyo Sambu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja inachangiwa kipande na barabara yetu ya TANROADS, pia kuna kipande ambacho wenzetu wa TARURA wanakifanya. Kwa upande wetu wa TANROADS tayari tumeshafanya usanifu na tunachofanya sasa hivi ni kuhakikisha kwamba hii barabara inapitika kwa muda wote wakati tukiendelea kutafuta fedha ili kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. FURAHA N. MATONDO K.n.y. MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: - Je, lini kipande cha barabara cha Kisorya hadi Nansio kitaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Spika, barabara ya kutoka Kokoto mpaka Mwandege ndiyo lango kuu la magari yanayotoka Kusini. Je, Serikali ina mpango gani wa kupanua barabara hiyo ili kupunguza msongamano?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Katika bajeti ambayo tumeitenga mwaka ujao na kweli nakubaliana kuna changamoto kubwa sana. Pale ambapo BRT II inaishia mwaka ujao tunaanza kutekeleza mradi wa kujenga kilometa 3.8 kwa barabara hizo nne, lakini mpango ni kwenda mpaka Vikindu kwa ajili ya kujenga hizo barabara nne kupunguza changamoto ya msongamano wa hizo barabara.

Name

Tabasamu Hamisi Hussein Mwagao

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Primary Question

MHE. FURAHA N. MATONDO K.n.y. MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: - Je, lini kipande cha barabara cha Kisorya hadi Nansio kitaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. TABASAM H. MWAGAO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi na mimi kuuliza swali la nyongeza na ni kwamba zimebakia siku nane leo kabla ya mwaka wa Serikali kuisha na Serikali ilikuwa imetueleza kwamba Sengerema tutafanya usanifu barabara ya Sengerema - Ngoma na Busisi - Ngoma kwa ajili ya lami kwenda Nyangh’wale na zimebakia siku nane hatujaona mkandarasi, Nini kauli ya Serikali Mheshimiwa Waziri?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara hii kwa sababu inaunganisha mikoa miwili wa Geita na Sengerema Mkoa wa Geita na Mkoa wa Mwanza sehemu kubwa inasimamiwa na Makao Makuu ya TANROADS ninataka nimuhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari Mhandisi Mshauri ameshapatikana kwa ajili ya kuanza kazi hii ya usanifu wa hii barabara.