Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 25 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 216 2022-05-18

Name

Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Primary Question

MHE. LUHAGA J. MPINA aliuliza:-

Je, ni vijana wangapi hawana ajira nchini na Serikali imewaandaaje kushindana katika soko la ajira ndani na nje ya nchi?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali namba 216 lililoulizwa na Mheshimiwa Luhaga Joelson Mpina kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, utafiti wa watu wenye uwezo wa kufanya kazi wa mwaka 2021 unaonesha kuwa vijana wa umri wa miaka 15 – 35 ni 17, 712,831 ambapo kati yao, vijana 14,219,191 wana uwezo wa kufanya kazi na vijana 3,493,640 hawana uwezo wa kufanya kazi kutokana na sababu mbalimbali kama vile masomo, ugonjwa na kadhalika. Kati ya vijana wenye uwezo wa kufanya kazi, vijana 12,486,682 sawa na asilimia 87.8 wana ajira na vijana 1,732,509 sawa na asilimia 12.2 hawana ajira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuhakikisha vijana wanaandaliwa ipasavyo kushindana katika soko la ajira, Ofisi ya Waziri Mkuu kwa maana ya Serikali imekuwa ikiandaa programu mbalimbali za kuweza kuhakikisha kwamba kunakuwa na mikakati ya kuwapatia vijana fursa za ajira na kuwaandaa kuweza kupata fursa ikiwemo mafunzo mbalimbali kwa maana ya uzoefu kazini, internship kwa hitimu wa vyuo vikuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo imekuwa na scheme mbalimbali ya kuweza kuwapatia mikopo, mafunzo, ya utarajali na mafunzo ya kilimo cha kisasa kutumia teknolojia ya vitalu nyumba kupitia mafunzo haya, zaidi ya vijana 84,245 wamenufaika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi ya Waziri Mkuu imeendelea kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Elimu pia Wizara ya Kilimo, kuweza kuhakikisha zinatolewa program mbalimbali ikiwa ni pamoja na mikopo, mafunzo na kutengeneza fursa mbalimbali zaa jira kutokana na Wizara hiyo.