Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Primary Question

MHE. LUHAGA J. MPINA aliuliza:- Je, ni vijana wangapi hawana ajira nchini na Serikali imewaandaaje kushindana katika soko la ajira ndani na nje ya nchi?

Supplementary Question 1

MHE. LUHAGA J. MPINA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa hili tatizo la ajira ni tatizo kubwa sana hapa nchini hivi sasa. Je, kwanini Serikali isifanye tracer study na kuandaa database ya vijana wote wanaohitimu mafunzo ili kuweza kuwatambua, kuweza kuwafuatilia na kujua namna nzuri ya kuwapatia ajira Serikalini pamoja na sekta binafsi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwanini Serikali isiandae mfumo mzuri wa kuwakopesha hawa vijana, wale wanaotaka kuingia kwenye ujasiriamali hata walau mtaji wa Milioni 20 wa kuanzia na wakajidhamini kwa vyeti vyao vya vyuo? (Makofi)

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Mweyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Luhaga Joelson Mpina kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kumekuwa na tatizo la ajira lakini kwa sehemu kubwa Serikali imeweza kulifanyia kazi Serikali ya Awamu Sita ya Mama Samia Suluhu Hassan. Tumekuwa na mikakati mingi ya kuweza kuhakikisha tatizo hili linapungua, mojawapo kwanza amefungua private sector kwa kubadilisha sheria pamoja na sera. Sambamba na hilo katika maeneo mengi vijana sasa wameanza kupata ajira kwenye miradi mikuwa ya maendeleo, lakini sambamba na hilo wameendelea kutoa ajira katika Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili katika kutafuta kanzidata, ni kweli tumekuwa katika kila nafasi ambazo zinatolewa kwa ajili ya ajira majina yale ambayo wamekuwa waombaji tumekuwa tukiyachukua kupitia kitengo cha ajira TAESA ili kuweza kupata takwimu sahihi za vijana ambao wamemaliza Vyuo Vikuu. Sambamba na hilo hatuwaachi hivyo, kumekuwa na mafuzo mbalimbali ya kuwapa internship, wapo vijana ambao wamepelekwa TRA na taasisi nyingine nyingi za Serikali kuweza kupata mafunzo ya uzoefu kazini sambamba na kuanzisha pia utaratibu wa kuwauhisha wale ambao wamehitimu kwenye vyuo mbalimbali vikiwemo vya VETA na FDC.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika eneo hilo hilo tumekwishakuanza kufanya, tumemaliza manpower survey kuweza kujua, lakini tunaenda kwenye hatua mbili sasa ya kufanya labour survey kuweza kujua idadi ya vijana ambao wanaweza kufanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili kuhusiana na mikopo, Serikali hii imekuwa ikitoa mikopo ya Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan tena kwa upendo mkubwa, ukiangalia hakuna kijana yoyote ambaye hapati mkopo, kumekuwa na scheme za utoaji mikopo katika elimu. Kwa mfano, kwa Shule za Msingi, tumekuwa tukitoa elimu bila malipo, lakini akimaliza sekondari anaenda Chuo Kikuu anakutana na bodi ya mikopo ambayo inampa mikopo, akitoa Chuo Kikuu, anapokuja nje anaenda kwenye Halmashauri zetu tunatoa mikopo ya 4:4:2 kwa maana ya asilimia Nne (4) kwa wanawake, asilimia Nne (4) kwa vijana na asilimia Mbili (2) kwa watu wenye ulemavu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zaidi ya hapo tumekuwa na scheme nyingine za makubaliano na mabenki mbalimbali kuweza kushusha riba na kutoa mikopo ikiwemo benki hizo za kilimo ambazo tayari zimekwishaanza kutoa na yalikuwa ni maelekezo mahususi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu kuweza kuhakikisha katika kila Halmashauri wanatenga maeneo maalum ya vijana kwa ajili ya kufanya kilimo na wanapewa mikopo kupitia Benki lakini pia Halmashauri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge pia Mheshimiwa Luhanga Mpina ambaye ndiye muuliza swali kama mtapitisha bajeti ya Wizara ya Kilimo, kule kuna mpango wa building the better tomorrow ambao unaenda kugusa vijana zaidi ya Milioni Moja katika kuhakikisha wanatengenezewa scheme za maeneo ya kilimo kwa maana ya block farming na wajibu wa Wizara ya Kilimo, itakuwa ni kuandaa kwanza maeneo hayo lakini pili kutafuta fecha kwa ajili ya kuwapa vijana hao na kuweka miundombinu na tatu ofisi ya Waziri Mkuu itakuwa wajibu wa kuweza kuratibu shughuli hizo. Kwa hiyo, Mheshimiwa hayo tumeyaona kwa kweli vijana wakae tu mkao wa kula na watoe ushirikiano kwa Serikali ya Mama Samia Suluhu Hassan inawaona na inawaangazia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zaidi ya hapo Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan hivi juzi, ametoa zaidi ya Shilingi Milioni 10 kila Mkoa kwa ajili ya wamachinga. Kwa hiyo, vijana wengi wako kwenye eneo hilo, ahsante. (Makofi)

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. LUHAGA J. MPINA aliuliza:- Je, ni vijana wangapi hawana ajira nchini na Serikali imewaandaaje kushindana katika soko la ajira ndani na nje ya nchi?

Supplementary Question 2

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa nafasi hii naomba nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, iko dhamira ya Serikali ya kutoa ajira kwa vijana hasa kupitia vitalu nyumba, lakini vitalu nyumba hivi ni ghali sana. Je, Serikali iko tayari sasa kuweka ruzuku katika vitalu nyumba ili vijana wengi waweze kujiajiri kupitia eneo hilo?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Massare, kama ifuatavyo:

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tumekuwa na programu ya kutoa elimu kwa ajili ya vijana kujifunza utengenezaji wa vitalu nyumba na tumekwishakufanya katika Halmashauri zaidi ya 82 na katika hayo maeneo ilikuwa wajibu wa kwanza ni kuhakikisha kwamba elimu inatolewa, lakini pia fedha na gharama zote zinaratibiwa na Serikali ya Mama Samia Suluhu Hassan kupitia ofisi ya Waziri Mkuu. Ni kweli kitalu nyumba kimoja kilikuwa kinagharimu zaidi ya karibia shilingi milioni 12, baada ya kuliona hilo na kwa ushauri mzuri wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria na muuliza swali Mheshimiwa Massare akiwa mjumbe tulitembelea Zanzibar na tuliweza kuona kwamba kuna uwezekano wa kutengeneza vitalu nyumba bila kutumia mabomba ya chuma na kutumia tu vitu vya asili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tumekwishakuanza kuwa-engage wataalam kuweza kutusaidia zaidi namna gani watashusha gharama na kutafuta wadau wengine ambao watasaidia katika kuweza kuwapa mikopo vijana hawa katika maeneo haya. Kwa kweli eneo hili limeonekana linapokelewa vizuri na vijana, tutahakikisha kwamba kwa ushirikiano na ushauri ambao mnautoa tutaufanyia kazi kila wakati. (Makofi)

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUHAGA J. MPINA aliuliza:- Je, ni vijana wangapi hawana ajira nchini na Serikali imewaandaaje kushindana katika soko la ajira ndani na nje ya nchi?

Supplementary Question 3

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Naibu Waziri kwa jinsi ambavyo unaeleza ni kama vile uko nje ya Tanzania. Tuna vijana wengi sana wamekosa ajira zaidi ya miaka sita sasa, lakini unasema kule chini kuna nafasi kwenye Halmashauri za wao kupata fedha, ninafahamu kuna ile 4.4.2 kama ulivyosema, lakini mwisho wa siku vijana wengi mfumo unawaacha nje kwa sababu hawana sifa za kupata mikopo hiyo?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwakagenda kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba wako vijana wengi ambao kwa wakati huo na kwa jinsi alivyosema ameshindwa kutueleza takwimu hasa, Serikali tunazo takwimu za vijana hawa, tumeshafanya Manpower survey, lakini wale wote wanaofanya application ya ajira, Vyuo Vikuu vyote tumekuwa tukipata taarifa za ajira na demographic population ya wanafunzi ambao wanamaliza Vyuo Vikuu at least kila mwaka. Tunao vijana zaidi ya Laki Mbili wanaoingia kwenye soko la ajira kutoka vyuo mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ya takwimu nikuambie Mheshimiwa ninazo za kutosha hapa na tutakueleza Serikali inawajali vijana kwa kiwango gani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, tunayo mifumo na programu ambazo tunaziandaa, labda programu ya kwanza nikikupa tu kwa faida yako tu Mheshimiwa uweze kujua na mengine nitakushirikisha ili tuwasaidie vijana kwenye eneo ni pamoja na hiyo internship ambayo inatusaidie siyo tu katika kuwafanya kupata mafunzo kazini, pia inawasaidia vijana hawa kuweza kuangaliziwa ajira ndani ya nje ya nchi kupitia wakala mbalimbali wa ajira waliosajiliwa na Ofisi Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo pia tumekuwa tukiendelea kuhakikisha tunatoa mikopo. Kwa hiyo, takwimu zipo, zaidi ya bilioni 150 zimekwishatolewa kwa vijana mbalimbali. Kwa hiyo, kama kuna vijana ambao wapo, labda pengine siyo Watanzania ni Wakenya, utanisaidia ili niweze kuwaingiza hapa na kuweza kuona ni namna gani tunawasaidia. Kwa hiyo, ninakutaarifu tu kwamba nipo Tanzania na huu ndiyo utaratibu wa Serikali ya Mama Samia Suluhu Hassan, Serikali ya takwimu na utekelezaji na Serikali inayowapenda vijana. (Makofi)