Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 25 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 221 2022-05-18

Name

Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza:-

Je, Serikali imejipangaje kuingia mikataba mipya isiyo na dosari kwani Mwaka 2024 ndio mwisho wa mkataba wa Songas?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jesca David Kishoa, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkataba kati ya Serikali na Kampuni ya Songas utaisha muda wake mwezi Julai, 2024. Ili kuhakikisha kwamba Serikali inakuwa na mkataba usiokuwa na dosari, Serikali haitaongeza muda wa mkataba utakaoishia mwezi Julai, 2024. Badada yake, Serikali itajadili mkataba mpya na iwapo pande zote zitakubaliana, mkataba mpya wenye tija kwa Taifa na usiokuwa na dosari utasainiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari Serikali kupitia TANESCO imeunda timu ya kupitia masuala ya msingi ya kuzingatiwa kwenye mkataba mpya kwa ajili ya maslahi kwa Taifa.