Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza:- Je, Serikali imejipangaje kuingia mikataba mipya isiyo na dosari kwani Mwaka 2024 ndio mwisho wa mkataba wa Songas?

Supplementary Question 1

MHE. JESCA D. KISHOA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza kabisa kwa dhati ya moyo wangu napenda kuchukua fursa hii kuipongeza Serikali kwa nia yake ya kutaka kusitisha Mkataba huu mwaka 2024 ni jambo ambali nimelipigia kelele kwa muda mrefu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya nyenzo muhimu sana na mahsusi kwa ajili ya kusaidia kutoingia mikataba ambayo haina tija katika Taifa ni pamoja na utekelezaji wa Sheria ya Tanzania ya Extractive Industry ya mwaka 2015 inayotaka mikataba yote ya sekta ya uzidiwaji kuwekwa wazi. Nataka kujua ni kwa nini kumekuwa kuna kusuasua kwa Sheria hii kutekelezeka?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili. Mkataba kati ya Serikali na Kampuni ya Songas ulioingiwa mwaka 2004 ni mkataba ambao unanyima fursa ya nchi ya Tanzania kunufaika na rasilimali kikamilifu. Nataka kujua Serikali imejipangaje mwaka 2024 kwenye mkataba mpya kuhakikisha kwamba hawafanyi makosa yaleyale kwenye eneo ya Investment cost, shareholding structure agreements na pamoja na eneo la capacity charges?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Jesca Kishoa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninapokea pongezi alizozitoa kwa Serikali kwa jitihada ambazo zinafanyika pia ninamshukuru kwa kuuliza maswali ya msingi kabisa yenye ufuatiliaji na tija kwa watu wote wa Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na swali la pili kwamba Serikali imejipangaje. Kama nilivyosema kwenye jibu la msingi, tayari imeshaundwa timu ya kuanza kupitia mkataba uliopo sasa na kubaini ni wapi tuliteleza na kutibu hayo maeneo ambayo tuliteleza ili yasijitokeze tena.

Mheshimiwa Mwenyekiti, timu zipo nyingi, ipo timu iliyoundwa na TANESCO inaendelea na upitiaji, ipo timu iliyoundwa na Wizara inaendelea na upitiaji, ipo timu iliyoundwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali inaendelea na upitiaji. Kama tulivyosema kwenye swali la msingi mkataba unaisha Julai, 2024 na hii ni Mei, 2022, kwa hiyo tuna miaka miwili kufikia muda wenyewe wa kuisha kwa mkataba. Tunayo imani kwamba tutakuwa tumeshajipanga vizuri na kuona ni kitu gani tutakifanya kuhakikisha kwamba mikataba tutakayoingia itatupa tija sisi kama Taifa na kuhakikisha kwamba nia na azma ya kupeleka umeme kwa wananchi inafikiwa kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye swali la kwanza la msingi la kwamba uwazi unakuwa guaranteed kiasi gani na Serikali. Niseme kama alivyosema kwenye Sheria ya Transparent Initiative ya Extractive Industry na umoja tuliokuwa taasisi tuliyokuwa nayo ya TEIT ambayo inasimamia uwazi na uwajibikaji katika mikataba hii, imekuwa ni shughuli inayoendelea nasi tunaji-subject kule kuweka mambo yetu wazi, kuonyesha wachimbaji au wadau katika eneo hilo wamekusanya pesa kiasi gani, wamepata faida kiasi gani, wamelipa kodi kiasi gani, tunaweka wazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kupitia Bunge hili Kamati za Kudumu za Bunge zimekuwa zikiitisha mikataba hii, zimekuwa ziikitisha value for money areas, zimekuwa zikiitisha Wizara na maeneo mbalimbali kwenda kueleza kwao na kujua namna gani haya mambo yako wazi. Kupitia Bunge hili tunaamini wananchi wote sasa wanakuwa tayari kuona kwamba Serikali inafanya kitu gani kwa uwazi na uwajibikaji kupitia sisi Wabunge ambao tunakuwa kwenye Kamati mbalimbali. Kwa hiyo, niseme hata yeye Mheshimiwa Mbunge yuko na uhuru kupitia kwenye Kamati kuweza kupata taarifa mbalimbali zilizopo katika maeneo hayo. (Makofi)

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza:- Je, Serikali imejipangaje kuingia mikataba mipya isiyo na dosari kwani Mwaka 2024 ndio mwisho wa mkataba wa Songas?

Supplementary Question 2

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Nimemsikia Mheshimiwa Naibu Waziri anasema Serikali iko tayari kupitia mkataba tu ambao ameusema Mheshimiwa Jesca Kishoa. Lakini Wizara yenu ina changamoto nyingi tu ya mikataba mbalimbali ambayo inahusaina na umeme na inailetea hasara Taifa hili, ikiwepo ule wa Pangea na Mgodi wa Geita na maeneo mengine. Hamuoni kwamba kuna haja sasa kama Serikali kupitia mikataba yote ili kuona tumekosea wapi huko tunakoenda nchi yetu isipate hasara na iweze kurekebisha sasa hivi, ukiwepo na mkataba wa Bwawa la Mwalimu Nyerere? Ahsante.(Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ester kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, mawazo na maoni yaliyotolewa kwa niaba ya Serikali niseme ninayachukua, tutaendelea kushirikiana Serikalini kwa ajili ya kushauriana namna bora ya kuweza kuwa tunafikia mikataba yenye tija kwa watu wote. Ile ambayo itakuwa imekwisha tutahakikisha tunafanya vizuri zaidi kwa nyakati zilizopo na ambayo inaendelea tutaona namna bora zaidi ya kuifanya iwe na tija kwa watu wote.