Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 25 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 222 2022-05-18

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itapeleka gari Kituo cha Polisi Muhange Wilayani Kakonko?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Josephine Johnson Genzabuke, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na mahitaji makubwa ya kibajeti, kwa sasa Serikali haitaweza kuvipatia vituo vyote vidogo vya polisi magari. Hivyo, kituo kidogo cha Polisi cha Muhange ambacho kipo Wilaya ya Kakonko kitaendelea kuhudumiwa na Kituo cha Polisi cha Wilaya ambacho kina magari mawili namba PT 1983 na PT 3631 Toyota Land Cruiser kama inavyofanyika kwa vituo vingine vidogo vilivyoko Wilaya ya Kakonko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.