Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka gari Kituo cha Polisi Muhange Wilayani Kakonko?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza. Kituo cha Muhange kipo mahali ambapo lipo soko la Ujirani Mwema na mara nyingi hutokea uhalifu na kutokana na ukosefu wa gari, Maaskari wa eneo hilo hulazimika kuazima pikipiki kwa Diwani wa eneo hilo. Ni lini sasa Serikali itapeleka japo pikipiki kwenye Kituo hicho? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili. Kituo cha Kitanga katika Wilaya ya Kasulu kiko mpakani, eneo hilo linatenganishwa na Mto Malagalasi, ukitoka Kitanga kwenda Malagalasi unavuka Mto Malagalasi. Kwa hiyo naangalia ni jinsi gani kuna umuhimu wa kupeleka gari katika eneo hilo, na eneo hilo, kutoka Kitanga kwenda Kasulu Mjini ni kilomita 150, katika eneo hilo hutokea ujambazi mara nyingi.

Ni lini sasa kwa umuhimu wa eneo hilo Serikali itapeleka gari ili kunusuru maisha ya wananchi? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Genzabuke kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Genzabuke kwa kufuatilia kwa karibu sana masuala ya usalama katika Mkoa wa Kigoma na hususani katika hizo Wilaya alizozirejea Kankonko na Kasulu. Hata hivyo nimjibu tu kwamba tumpongeze Mheshimiwa Diwani kama moja ya wadau aliyetoa vyombo vya usafiri kama pikipiki na kama ambavyo Mkurugenzi wa Wilaya ya Kankonko pia ameahidi kutoa pikipiki ili kusaidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumezungumza hapa kwamba Wizara kupitia Jeshi la Polisi itapata magari zaidi ya 300 ifikapo mwezi Septemba na maeneo yenye changamoto kubwa za kiusalama kama haya ya mipakani yatapewa kipaumbele. Kwa hiyo nimuondoe shaka Mheshimiwa Genzabuke. (Makofi)

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka gari Kituo cha Polisi Muhange Wilayani Kakonko?

Supplementary Question 2

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Wilaya ya Mkoani, Mkoa wa Kusini Pemba ina vituo Vinne vya Polisi ambavyo vina gari moja ambalo lilipatikana mwaka 1980. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapelekea gari nyingine? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema kwenye majibu wakati najibu swali la msingi kwamba tunao mpango wa kuimarisha usafiri kwenye maeneo yote ambayo yana changamoto ya usafiri ikiwemo Mkoa wa Kusini Pemba. Kwa hiyo, kulingana na vipaumbele na mahitaji ya magari, magari tutakayoyapata mapema iwezekanavyo yale 78 Mkoa wa Kusini Pemba pia utazingatiwa. (Makofi)

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka gari Kituo cha Polisi Muhange Wilayani Kakonko?

Supplementary Question 3

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Msalala, Halmashauri ya Msalala ina Kituo cha Wilaya na haina gari la Polisi. Kama unavyofahamu kwenye maeneo yetu ya uchimbaji usalama ni hatari sana ukizingatia kwamba kwa sasa kumeanza kuibuka makundi mbalimbali. Sasa ni lini Serikali itachukua hatua za dharura wakati ikisubiria mpango wa kuleta magari yale mengine, ichukue hatua ya dharura ili kuhakikisha kwamba wanatupatia gari la Polisi tuweze kukabiliana na uhalifu katika eneo hilo?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Iddi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua ni kweli kwamba maeneo ya migodi ni maeneo yanayovutia pia matendo ya uhalifu. Kwa hiyo tutakaa na Mheshimiwa Mbunge ili tukae na RPC wa Mkoa wa Shinyanga kuona kama pana magari ya ziada basi sehemu ya magari yale yahamishiwe kwenye Wilaya hii ya Kahama ili kuimarisha usafiri kwenye eneo hilo. (Makofi)