Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 26 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 224 2022-05-19

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango wa kuhakikisha vijiji vyote vya Mkoa wa Songwe vinapata umeme wa REA?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stella Simon Fiyao, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Songwe una jumla ya vijiji 307; vijiji 180 vina umeme na vijiji 127 havijafikiwa na miundombinu ya umeme. Vijiji hivyo 127 ambavyo havijafikiwa na miundombinu ya umeme vinanufaika kupitia mradi wa REA III mzunguko wa pili unaoendelea. Utekelezaji wa mradi unaendelea na Mkandarasi Derm Electrics ndiye anayetekeleza mradi kwa kipindi cha miezi kumi na nane kwa gharama ya shilingi bilioni 11.23. Mradi huu unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2022.