Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango wa kuhakikisha vijiji vyote vya Mkoa wa Songwe vinapata umeme wa REA?

Supplementary Question 1

MHE. STELLA S. FIYAO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri, lakini naomba niwe na swali la nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Wizara imekuwa na utaratibu wa kufikisha huduma katika makao makuu ya vijiji na kusababisha watu wa vitongoji kukosa huduma.

Je, ni lini Wizara hii itaanza kufikisha huduma hii kwenye vitongoji ili wananchi wengi waweze kufikiwa na huduma hii ya Umeme? Nashukuru sana. (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Stella Simon Fiyao, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba hatua ya kupeleka miundombinu ya umeme kwenye maeneo yote ya vijiji imekuwa ikienda awamu kwa awamu, ni kwamba tulianza na vijiji kidogo kulingana na uwezo wa Serikali uliokuwepo, lakini baadaye Serikali ikajihimu na kuhakikisha vijiji vyote vinafikishiwa miundombinu ya umeme angalau kwa kuanza na makao makuu ya vijiji. Lakini ipo mipango ya Serikali madhubuti kabisa ya kuhakikisha kwamba kila eneo linafikiwa na umeme na njia hizo ni kwa kuanza na miradi yetu ya ujazilizi inayoitwa densification ambapo tuna ya kwanza, ya pili na ya tatu zinaendelea, na zitaendelea kufanyika kwa kadri ya upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Spika, lakini Serikali imeona ni vema kutafuta fedha nyingi kwa wakati mmoja na kumaliza vitongoji vyote ambavyo havijafikiwa na umeme na kama ambavyo tumeshasema mara kadhaa hapa Bungeni tumeona kwamba tunahitaji takribani shilingi trilioni sita na bilioni kama mita tano ili kumaliza maeneo yote ya vitongoji na Serikali ipo katika harakati za kuhakikisha kwamba inapata fedha hii kufikisha umeme katika maeneo hayo, lakini katika kipindi hiki cha kuanzia fedha inapopatikana Serikali inazidi kusogeza miundombinu ya umeme katika vitongoji kwenye maeneo yetu. (Makofi)

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango wa kuhakikisha vijiji vyote vya Mkoa wa Songwe vinapata umeme wa REA?

Supplementary Question 2

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mbulu Vijijini kuna vitongoji 400 na vijiji 76; ulifika Mheshimiwa Waziri ukatoa ahadi vijiji vyote vitapata umeme.

Je, ni lini ahadi yako inatekelezwa? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Flatei Massay kama nilivyojibu swali la msingi kwamba kadri Serikali inavyoendelea kupata fedha itajitahidi kuhakikisha kwamba vitongoji vyote vinapatiwa umeme katika muda mfupi ujao.

Name

Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango wa kuhakikisha vijiji vyote vya Mkoa wa Songwe vinapata umeme wa REA?

Supplementary Question 3

MHE. AGNES M. MARWA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana; Mkoa wa Mara ni kati ya Mikoa iliyokaa kimkakati ukizingatia ni Mkoa uliomtoa Muasisi Mwalimu Julias Kambarage Nyerere.

Je, ni lini Serikali itapeleka Umeme wa REA katika vijiji vyote vya Mkoa wa Mara ukizingatia wakati wakiomba kura Mama yetu Samia Suluhu Hassan na Hayati Magufuli waliahidi kwamba vijiji vyote vilivyobaki vitapata umeme?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Agnes Marwa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hivi tunavyozungumza mradi kabambe wa kupeleka umeme kwenye vijiji unaoitwa REA III Round Two unaendelea katika vijiji vyote nchini, na Mkoa wa Mara ni mmojawapo kati ya maeneo hayo. Na ninakumbuka mkandarasi anayepeleka umeme katika maeneo haya anaitwa Giza Cables, anapeleka umeme katika Mikoa ya Manyara na Mara, na tunatarajia kufikia Desemba mwaka huu vijiji vyote ambavyo havijafikiwa na miundombinu ya umeme vitakuwa vimefikiwa na umeme kwa mkataba tuliokuwa nao na tunasimamia kwa karibu kabisa kwa sababu pesa tunayo na kazi inaendelea.

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango wa kuhakikisha vijiji vyote vya Mkoa wa Songwe vinapata umeme wa REA?

Supplementary Question 4

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Spika, katika vijiji ambavyo vilipatwa na changamoto ya umeme kutokukamilika ni vijiji takribani vyote vya kata kama tatu hivi katika Jimbo la Lulindi; Kata ya Mchauru kulikuwa na hiyo; Kata ya Sindano, Kata ya Luatala.

Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha vijiji hivi vilivyokosa umeme mpaka sasa hivi katika kata hizo na maeneo mengine ya Lulindi vinapata umeme?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mchungahela kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nikwamba ifikapo Desemba, 2022 Serikali imeji-commit kuhakikisha inafikisha miundombinu ya umeme katika vijiji vyote Tanzania Bara ambavyo havijafikiwa na umeme na kazi zinaendelea katika maeneo mbalimbali, wakandarasi wako site wanaendelea.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango wa kuhakikisha vijiji vyote vya Mkoa wa Songwe vinapata umeme wa REA?

Supplementary Question 5

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa kuwa katika Jimbo la Vwawa kuna vijiji 31 ambavyo bado havina umeme, na kwa kuwa mkandarasi sasa hivi karibu mwaka mmoja umekatika hakuna kijiji hata kimoja ambacho kimepata umeme.

Je, Serikali inatuhakikishiaje kwamba kufikia Desemba vijiji vyote hivyo vitakuwa vimewashwa umeme?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Japhet Hasunga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, taratibu za kupeleka umeme wa REA na miradi mingine mikubwa uko katika awamu tofauti tofauti na kwa harakaharaka tunayo awamu ya kumpata mkandarasi na tukishasaini mkataba anakwenda site kufanya physical verification, anakwenda kukagua maeneo na kuona uhalisia wake, lakini tunarudi mezani yeye pamoja na TANESCO na REA kuangalia na kukubaliana scope ya kazi yenyewe ambayo inatakiwa ifanyike halafu anakwenda kwenye hatua ya tatu ya kuagiza vifaa na hatua ya nne ni ya kwenda site na kuanza kufanya kazi.

Mheshimiwa Spika, ninaamini kabisa kwa Mheshimiwa Japhet Hasunga mojawapo au mbili au tatu ya hatua hizo zinaendelea, na tunatarajia ifikapo Desemba muda wa kufanya kazi kwa miezi hii sita, saba iliyobakia tutakabana na wakandarasi kuhakikisha kwamba tunafikisha huduma hii ya umeme kwenye maeneo yote kwa sababu tayari vifaa vimeshanunuliwa na surveys zilishafanyika na sasa wako site wanaendelea kufanya kazi, kwa hiyo kazi zitakamilika. (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango wa kuhakikisha vijiji vyote vya Mkoa wa Songwe vinapata umeme wa REA?

Supplementary Question 6

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kule kwenye Jimbo la Tarime Vijijini eneo la Nyamungo na Nyamwaga wananchi wangu wamekwenda kulipia nguzo za umeme wa REA badala ya kulipia shilingi 27,000 wamedaiwa shilingi 515,000 kwa nguzo moja.

Naomba nipate kauli ya Serikali kwamba bei imebaki shilingi 27,000 ile ambayo tulikubaliana kwa wananchi wetu au kuna mabadiliko mengine sasa ya gharama ya umeme wa REA? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwita Waitara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, bei za umeme za maeneo ya vijijini ni shilingi 27,000 bila kujali habari ya nguzo au transfoma au nini; kwa vijijini ni shilingi 27,000. Maeneo ya mijini ndiyo yamerudia kwenye zile bei ambazo tayari Serikali inaweka ruzuku ili ziweze kuwa za chini kidogo ili wananchi waweze kuzikimu, lakini kwa vijijini ni shilingi 27,000.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango wa kuhakikisha vijiji vyote vya Mkoa wa Songwe vinapata umeme wa REA?

Supplementary Question 7

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya cha Bakorongo kilikamilika na kufunguliwa na Rais wa Awamu ya Nne, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, mwaka 2007, tangu hapo maelekezo yamekuwa yakitolewa kiwekewe umeme na hakijawekewa.

Mheshimiwa Spika, nataka kujua nini kauli ya Serikali kuhusu kuweka umeme katika kituo hicho cha afya? Ahsante.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tunayo maeneo mengi ya taasisi za umma ambayo hayajafikiwa na umeme, kwenye vituo vya afya, vyanzo vya maji, shule na taasisi za dini. Baada ya kuona mahitaji makubwa wenzetu wa REA wamekuja na mkakati na mradi maalum ambao tutapeleka umeme katika vyanzo vya maji, vituo vya afya na migodi ili kuharakisha na kurahisisha ufikaji wa miundombinu ya umeme katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, naomba baada ya kutoka hapa basi nizungumze na Mheshimiwa Mbunge ili tuone kama liko captured kwenye huo mradi wetu ambao tunatarajia unaweza ukaanza mwishoni mwa mwaka huu. (Makofi)

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango wa kuhakikisha vijiji vyote vya Mkoa wa Songwe vinapata umeme wa REA?

Supplementary Question 8

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Tarafa nzima ya Mungaa katika Jimbo la Singida Mashariki nilishasema hapa haina umeme hata kijiji kimoja. Lakini juhudi zilifanyika, kata nne zimeshawekewa nguzo leo ni mwezi wa nne unakwenda wa tano.

Ni lini sasa mkandarasi atarudi kuja kuweka nyaya na transfoma ili wananchi wale waanze kupata umeme wakati wengine wanasubiria kumalizia nguzo zilizobaki?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mtaturu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kulitokea changamoto ya ongezeko la bei, hasa kwenye bidhaa za vyuma, copper na aluminium ambazo zinatumika kutengeneza transfoma, nyaya na accessories nyingine katika uunganishaji wa umeme.

Katika kujadili tatizo hili na kulitatua imetuchukua kidogo muda, lakini tunakaribia kumaliza jambo hili na tunaamini mwishoni mwa mwezi huu basi habari ya kuvuta waya, kufunga transfoma na mengine yataendelea kwenye maeneo ambayo tayari nguzo zilishasimamishwa. Na ninaelekeza kwa wakandarasi yale maeneo ambayo bado nguzo hazijasimama basi kazi zisizohusika na ongezeko la bei ziendelee kufanyika wakati mambo mengine haya yakiendelea kukamilika, kuhakikisha kwamba umeme unafika kwa wakati.

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango wa kuhakikisha vijiji vyote vya Mkoa wa Songwe vinapata umeme wa REA?

Supplementary Question 9

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Spika, Jimbo la Geita Mjini kata nane hazijafikiwa na umeme mpaka leo. Serikali iliahidi kwamba kutakuwa na mradi wa peri urban ambao ungeanza mwezi Aprili, lakini leo ni mwezi Mei mradi huo haujaanza. Ni lini mradi huo utaanza?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Constantine Kanyasu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kuna maeneo ambayo yako mijini lakini yana muonekano wa kuwa vijijini, ukiachana na kwake Geita, hata Jimbo ninalotoka mimi la Bukoba Mjini lina hali hiyo hiyo; na ni kweli Serikali iko katika harakati za mwisho za kukamilisha Mradi wa peri urban ambao tunatarajia utaanza kufikia mwezi Julai ili kupeleka umeme katika maeneo ya mijini, lakini yenye muonekano wa vijiji.

Nimuombe Mheshimiwa Mbunge awaambie wananchi wavumilie kidogo, Serikali ya Awamu ya Sita itatimiza ahadi yake na mimi nimo humohumo.

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango wa kuhakikisha vijiji vyote vya Mkoa wa Songwe vinapata umeme wa REA?

Supplementary Question 10

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kuniona.

Mheshimiwa Spika, kata tatu za Kilolo yaani Ukwega, Nyanzwa na Udekwa, hazina umeme, na mkandarasi alikuja akachomeka nguzo, sasa ni miezi sita haonekani.

Je, Serikali iko tayari kumuita na kumtafuta huko aliko ili aende akamalizie ile kazi kule? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nyamoga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli eneo moja na eneo lingine hatua za utekelezaji zinatofautiana kulingana na mkandarasi alianza lini na amepata vifaa wapi na mambo kama hayo na kama nilivyoelekeza wakandarasi wote waendelee na kazi zisizohusiana na mazungumzo tunayoyafanya kuhusiana na bei.

Mheshimiwa Spika, naomba nikitoka hapa niwasiliane na Mheshimiwa Nyamoga ili nione hasa kwake kuna changamoto gani mahususi ili kama ni kuitatua mara moja tuitatue, kama ni ile ambayo inaendelea kwenye taratibu nyingine basi namhakikishia kwamba kazi itaendelea na itakamilika kwa wakati.

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango wa kuhakikisha vijiji vyote vya Mkoa wa Songwe vinapata umeme wa REA?

Supplementary Question 11

MHE. FURAHA N. MATONDO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Serikali ilitangaza mabadiliko ya bei za umeme kwa wananchi wanaoishi mjini. Wananchi wanaoishi pembezoni mwa mji mfano Kishiri, Sangabuye, Buhongwa na Kayenze na tayari walishalipia umeme wa shilingi 27,000.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawekea umeme? Walishalipa kabla ya tangazo la Serikali? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kutoa majibu kwenye swali la nyongeza la Mheshimiwa Furaha kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba kusema maneno machache yenye uhalisia na ukweli; wale wote waliokuwa wamelipa shilingi 27,000 kabla ya mabadiliko ya bei wataunganishiwa umeme kwa gharama ya shilingi 27,000. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, agizo hili liko kwa Mameneja wote wa Mikoa na wa Wilaya na wanajua, na tulikubaliana kuwa wale wenzetu waliokuwa wametangulia kulipa wapewe kipaumbele kwa kufanya first in first out. Kwa hiyo wale ambao bado hawajaunganishiwa na walishalipa shilingi 27,000 wasiwe na wasiwasi gharama italipwa na wale ambao wanaona wamechukua muda mrefu naomba tuwasiliane ili tuweze kuona tatizo na changamoto iko wapi ili tuweze kuondokana na tatizo hili.