Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 26 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 227 2022-05-19

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Mkalama ambacho ni gofu la ghorofa kwa muda mrefu sasa ilhali Wilaya haina kituo chenye hadhi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Francis Isack Mtinga, Mbunge wa Iramba Mashariki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Polisi kinachojengwa katika Wilaya ya Mkalama ni Kituo cha Daraja A na ni cha ghorofa moja. Ujenzi wake umeanza Juni, 2015 na unatarajia kutumia jumla ya shilingi 792,450,000.00 hadi kumalizika kwake. Hadi sasa fedha zilizotumika ni shilingi 100,000,000.00 na kazi iliyobaki ni kumwaga silabu, kupaua na kazi za kumalizia. Katika mwaka ujao wa fedha 2022/2023 zimetengwa fedha kiasi cha shilingi 692,450,000 kwa ajili ya kumalizia kazi ya ujenzi wa kituo hicho. Nashukuru.