Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Mkalama ambacho ni gofu la ghorofa kwa muda mrefu sasa ilhali Wilaya haina kituo chenye hadhi?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS I. MTINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri sana ya Serikali ninamaswali mawili madogo ya nyongeza.

Kwa kuwa mfumo wetu wa bajeti niwakutumia kadri unavyokusanya. Je, na kwa sababu kituo hiki ni cha Wilaya na ni chamuhimu sana Waziri ananiambiaje kuhusu kunipa kipaumbele katika fedha za maendeleo za kwanza tu zitakazopelekwa katika bajeti inayoanza Julai? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa upya wa Wilaya ya Mkalama tuna askari 83 tu, tuna upungufu wa askari 57. Je, Waziri ananipa commitment gani kuhusu vijana askari wanaomaliza kozi muda mfupi ujao kupeleka katika Wilaya yangu? Ahsante. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mtinga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, moja; tunamuhakikishia kwamba fedha zilizotengwa katika mwaka wa fedha ujao shilingi milioni 992 tutahakikisha kwamba zinapelekwa katika jimbo lake ili kukamilisha kituo hicho kama kipaumbele miongoni mwa vipaumbele vilivyotajwa na Waziri wakati wa kuwasilisha bajeti yake.

Mheshimiwa Spika, pili; tunatambua kwamba wanao askari 84 na katika mgao wa askari wanaotarajia kumaliza mafunzo zaidi ya 4000 waliopo vyuoni Wilaya ya Iramba ni moja ya maeneo ambayo yatazingatiwa ili kuhakikisha kwamba wanapata askari wa kutosha, ahsante. (Makofi)

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Mkalama ambacho ni gofu la ghorofa kwa muda mrefu sasa ilhali Wilaya haina kituo chenye hadhi?

Supplementary Question 2

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kuniona.

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Polisi kilichopo Kata ya Keza Wilayani Ngara kilijengwa kwa nguvu za wananchi, lakini mpaka sasa hakijamalizika; je, ni lini Serikali itamalizia kituo hicho? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Oliver Semuguruka kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba wananchi wa Ngara wamejitahidi kujenga kituo hicho na tunampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji wake pamoja na Mbunge wa Jimbo la Ngara na ahadi yetu ni kwamba katika mwaka ujao vituo vya kumalizia kwa mujibu wa bajeti yetu ni 13, vituo vingine vitaendelea kupangwa kwa kipaumbele katika bajeti zinazofuata katika miaka ijayo huko mbele. (Makofi)

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Mkalama ambacho ni gofu la ghorofa kwa muda mrefu sasa ilhali Wilaya haina kituo chenye hadhi?

Supplementary Question 3

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, ahsante; Wilaya ya Kahama ina Halmashauri tatu ambapo kila Halmashauri mmeanzisha vituo vya Wilaya lakini vituo hivyo vya wilaya havina vituo vya polisi.

Sasa nataka kufahamu ni lini Serikali itaanzisha ujenzi wa kituo cha polisi nakwakuzingatia kwamba mimi Mbunge wao nipo tayari sasa kutoa tofali 4000 ili tuanze ujenzi huo haraka iwezekanavyo? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Iddi Kassim, Mbunge wa Kahama kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza tumpongeze kwa juhudi zake za kusaidia sekta ya usalama wa raia na mali zao kwa kuchangia idadi hii ya 4,000 ya matofali lakini mpango wetu ni kujenga vituo vya polisi vya Wilaya zile halmashauri ni kuimarisha tu kwa kuweka vituo vingine kwa hivyo kipaumbele kitakuwa kujenga kituo kikuu cha Wilaya ya Kahama na zile Halmashauri zitaendelea kuwekewa vituo visaidizi kwa ngazi ya tarafa na kata kama ambavyo sera yetu ya usalama wa raia inavyoelekeza. (Makofi)