Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 27 Water and Irrigation Wizara ya Maji 235 2022-05-20

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka maji katika Kata ya Katuma ambayo ndiyo inatunza chanzo cha maji cha Mto Katuma?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Moshi Selemani Kakoso, Mbunge wa Mpanda Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali inatekeleza mradi wa maji kwa kutumia visima virefu vinne na kazi zilizopangwa kutekelezwa ni pamoja na ujenzi wa matanki matano yenye ujazo wa lita 400,000, ujenzi wa vituo 25 vya kuchotea maji na mtandao wa bomba wenye urefu wa kilometa 30.4. Mradi huu unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Oktoba, 2022.

Mheshimiwa Mwenyekiti, chanzo cha Mto Katuma kinanufaisha wananchi wa Kata ya Katuma kwa shughuli za kilimo ambapo Serikali imetoa vibali vitano vya kutumia maji kwa skimu za umwagiliaji wa kilimo cha mpunga. Katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali itaajiri Mtaalam Mshauri wa kufanya usanifu wa mradi wa maji kwa kutumia chanzo cha maji cha Ziwa Tanganyika kupeleka Mkoa wa Katavi ambapo Wilaya ya Tanganyika itanufaika.