Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka maji katika Kata ya Katuma ambayo ndiyo inatunza chanzo cha maji cha Mto Katuma?

Supplementary Question 1

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza: Mradi wa Kata ya Katuma ulipata Mkandarasi HEMATEC ambaye aliingia mkataba wa kufanya kazi tarehe 14 Desemba, 2021, mpaka sasa Mkandarasi huyo hajawahi kufika kwenye eneo husika:-

Je, Serikali haioni sasa ni wakati wa kuchukua hatua za dharura ku-terminate huo mkataba ambapo kimsingi mradi huo unatakiwa ukamilike tarehe 20 mwezi wa Sita?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili: Tunapongeza jitihada zinazofanywa na Serikali na kuleta miradi mingi kwenye eneo la kwetu. Meneja wa RUWASA wa Wilaya ya Tanganyika hana gari la kumsaidia kufanya kazi:-

Je, ni lini Serikali italeta fedha au kuleta gari ili liweze kusaidia kutoa huduma kwenye eneo hilo? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu, maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Moshi Kakoso, Mbunge wa Mpanda Vijijini, kama ifutavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa, napenda kumpa pole Mheshimiwa Mbunge, amekuwa akifuatilia sana huyu Mkandarasi, lakini sisi kama Wizara hatutafumbia macho Mkandarasi yoyote mzembe, hata kama tumesaini mkataba, lakini ukienda kinyume na mkataba, tutakuweka pembeni kwa sababu hatuko tayari kufanya kazi na mtu anayetuchelewesha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo kwa kutumia Bunge lako Tukufu, naomba nitoe wito kwa ma-RM wote ambao Wakandarasi wao wanalalamikiwa kama huyu HEMATEC, RM wa eneo hili. Nitapenda ulete taarifa yako kesho asubuhi ili kujua ukweli wa suala la huyu Mkandarasi na endapo itabainika ni mzembe, tutamchukulia hatua stahiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na DM wa Tanganyika kupatiwa gari, utaratibu unaendelea. Tunashukuru sana utendaji mzuri wa Director General wa RUWASA, Eng. Clement Kivegalo, ameendelea kufanya taratibu za kuona ma-DM wote wanapata vyombo vya usafiri. Hivyo katika magari yatakayokuja, naamini DG ataweka pia msisitizo kwa eneo la Tanganyika kwa umuhimu wake.