Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 29 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 249 2022-05-24

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza:-

Je, ni lini Mji wa Geita utakuwa Manispaa kwa kuwa taratibu zote zimekamilika na imefikia viwango vya kupewa hadhi ya Manispaa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Constantine John Kanyasu, Mbunge wa Geita Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Ofisi ya Rais – TAMISEMI ilipokea mapendekezo ya kupandisha hadhi Halmashauri ya Mji Geita kuwa Manispaa. Mapendekezo hayo yalifanyiwa uhakiki na timu ya Wataalam Kutoka OR-TAMISEMI, kati ya vigezo 21 Halmashauri ya Mji wa Geita ilikuwa imekidhi vigezo 18 sawa na asilimia 85. Vigezo ambavyo havikuwa vimefikiwa na Mji wa Geita ni pamoja na kutokuwa na Mpango Kabambe wa uendelezaji Mji, eneo lililopimwa lisipungue asilimia 75 ya eneo lote kutofikia asilimia 75 zinazohitajika za wakazi waliokuwa wameunganishwa na huduma ya maji. Hivyo, Halmashauri hii haikuweza kupandishwa hadhi kwa kuwa ililazimu kukidhi vigezo vyote kwa pamoja kwa mujibu wa mwongozo wa kuanzisha maeneo ya utawala wa mwaka 2014 ili kupandishwa hadhi ya kuwa Halmashauri ya Manispaa.