Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza:- Je, ni lini Mji wa Geita utakuwa Manispaa kwa kuwa taratibu zote zimekamilika na imefikia viwango vya kupewa hadhi ya Manispaa?

Supplementary Question 1

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Kwanza ninasikitika kwamba majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri ni ya uwongo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mji wa Geita una master plan na ilizinduliwa na Mheshimiwa Waziri mwaka 2020 na zoezi hilo ni la siku nyingi zaidi ya miaka miwili na kitu iliyopita na Mji wa Geita umepimwa zaidi ya asilimia 70, kwa hiyo, kwa kuwa majibu yake ni ya uwongo, labda ni ulize tu swali.

Mheshimiwa Naibu Spika, moja, ni lini sasa wataenda kuangalia upya vigezo kwa sababu jibu alilokuja nalo siyo sahihi wataenda kuangalia upya vigezo vya kuupandisha Mji wa Geita kuwa Manisapaa?

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, Miji mingi iliyopanishwa kuwa Manispaa suala la vigezo vya kupimwa halikuwepo na iko Miji mikubwa kwa asilimia kubwa ni squater, hili sharti la kupimwa ni sharti jipya, ni lini wataliondoa sharti hilo?(Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili madogo ya nyongeza ya Mheshimiwa Constantine John Kanyasu, Mbunge wa Geita Mjini kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, tuna vigezo ambavyo Ofisi ya Rais, huwa tunaviweka, kupitia vigezo vyetu, hayo ni maeneo ambayo tulikwenda tukaikabidhi Halmashauri ya Mji Geita na tukawaeleza kwanini hawajatimiza hivyo vigezo. Tulikuwa tumeainisha moja ya mpango wa master plan, walikuwa wamepata Mkandarasi ambaye alikuwa bado hakumaliza hatua nne za mwisho kwa hiyo, kama wamemaliza sasa hilo linakuwa ni jambo lingine, lakini kabla ya hapo walikuwa hawajakidhi vigezo. Kwa hiyo, tumepokea wazo la Mheshimiwa Mbunge la kupitia upya hivyo vigezo, lakini kwa sasa hii ndiyo hali halisi ambayo iko chini kwenye ground.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho ni kwamba nia ya Serikali ni kuhakikisha manispaa au halmashauri zote ambazo zinakuwa na hadhi, zikikidhi vigezo, jukumu letu litakuwa ni moja tu kupeleka kwa mamlaka na mamlaka ndiyo itakuwa na uamuzi wa mwisho.

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza:- Je, ni lini Mji wa Geita utakuwa Manispaa kwa kuwa taratibu zote zimekamilika na imefikia viwango vya kupewa hadhi ya Manispaa?

Supplementary Question 2

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Makao Makuu ya Mikoa mingi yamepewa Manispaa. Nataka kufahamu ni lini Serikali itatupatia Manispaa katika Mkoa wa Songwe kwa maana ya Vwawa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Juliana Shonza, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Songwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali kama hili nililijibu siku ya jana, ambako nilisema Mbunge wa Jimbo la Vwawa, Mheshimiwa Japhet Hasunga. Nimhakikishie tu kwamba Mkoa wa Songwe ni moja kati ya Mikoa ambayo imeiomba kupewa hadhi ya kuwa na Manispaa, kinachofanyika sasa hivi ni kuhakikisha kwamba vile vigezo ambavyo vimewekwa vinapitiwa na wakishakidhi vile vigezo maana yake tutaishauri mamlaka iweze kama kuipatia ama yenyewe itaona vingenevyo. Kwa hiyo, huo ndiyo msimamo mpaka sasa wa Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.(Makofi)

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza:- Je, ni lini Mji wa Geita utakuwa Manispaa kwa kuwa taratibu zote zimekamilika na imefikia viwango vya kupewa hadhi ya Manispaa?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi, Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro iko katikati ya Majiji ya Dodoma, Arusha na Dar es Salaam. Je, ni lini Manispaa ya Morogoro itakuwa Jiji?

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Dkt. Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, endapo Manispaa ya Morogoro itakuwa imekidhi vigezo na itakuwa imefuata taratibu zote, jukumu letu kama Ofisi ya Rais, TAMISEMI, ni kufanya tathmini na kupeleka mapendekezo hayo kwa mamlaka ili iweze kufanya maamuzi. Ahsante.

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza:- Je, ni lini Mji wa Geita utakuwa Manispaa kwa kuwa taratibu zote zimekamilika na imefikia viwango vya kupewa hadhi ya Manispaa?

Supplementary Question 4

MHE. ENG. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Je, ni lini Serikali itapandisha Mamlaka ya Mji Mdogo wa Kateshi, kuwa Mamlaka kamili ya Mji wa Kateshi?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Eng. Samweli Mbunge kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunachohitaji katika Halmashauri yake ya Hanang’ ni kufuata tu vile vigezo halafu baada ya kumaliza hivyo vigezo watuletee nasi tutakuja kufanya tathmini tuone kama inakidhi ili tuweze kupandisha hadhi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza:- Je, ni lini Mji wa Geita utakuwa Manispaa kwa kuwa taratibu zote zimekamilika na imefikia viwango vya kupewa hadhi ya Manispaa?

Supplementary Question 5

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Kuna Mamlaka za Miji Midogo hapa nchini imekaa kwenye wadhifa huo kwa muda mrefu na sasa vinakidhi kwenda kwenye hatua nyingine. Je, ni lini Serikali sasa itazipandisha ikiwemo Mamlaka ya Mji Mdogo wa Karatu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKAO NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cecilia Paresso, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunatambua kwamba kuna mamlaka nyingi ambazo zinahitaji kupanda hadhi, moja ya jukumu kubwa la Serikali sasa hivi ni kuhakikisha kwanza tunaboresha miundombinu katika Halmashauri ambazo bado hazijakamilika. Lakini pili, kulingana na mahitaji tutapandisha hadhi, na sisi tutapendekeza kulingana na vilevile mahitaji ya wakati husika. Kwa hiyo, hilo ndiyo jibu la Serikali kwa sasa.