Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 29 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 250 2022-05-24

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-

Je Serikali ina mpango gani wa kuwaongezea zaidi posho Madiwani na kuwalipa mishahara Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Flatei Gregory Massay, Mbunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua kazi kubwa inayofanywa na Waheshimiwa Madiwani pamoja na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji katika kusimamia utekelezaji wa shughuli za maendeleo katika maeneo yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuzingatia hilo, Serikali inatafuta vyanzo vipya vya fedha ili kuongeza posho za Madiwani. Pamoja na hilo, Halmashauri kwa kutumia mapato yake ya ndani zinawajibika kutenga sehemu ya mapato hayo kwa ajili kuwalipa posho Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji.