Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Je Serikali ina mpango gani wa kuwaongezea zaidi posho Madiwani na kuwalipa mishahara Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji?

Supplementary Question 1

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza.

Kwa kuwa, Serikali imekiri kwamba inatafuta fedha kulipa Madiwani na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji na umeelekeza kwamba Halmashauri ifanye utaratibu huo. Je, uko tayari kuelekeza Halmashauri zote ili hela hizi zilipwe kwenye Mfuko Mkuu ili watu hawa wakapate kulipwa katika bajeti ya mwakani?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, tunampongeza Mheshimiwa Rais kwa sababu ameona na amesikia kilio cha wafanyakazi ameongeza asilimia 23 kwenye mshahara. Je, huoni kwamba sasa ndiyo muhimu kuona kwamba watumishi wengine na hasa hawa niliowataja kwenye asilimia hii wapo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Flatei Gregory Massay, Mbunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli na hili ni agizo kwa Halmashauri zote kuhakikisha sehemu ya mapato ambayo yanashuka kwenda katika vijiji ni sehemu ya posho ambazo wenyeviti wa vijiji wanapaswa kulipwa. Kwa hiyo, tutakachokifanya tu ni kufuatilia kuona agizo hili ama utaratibu huu unatekelezeka.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili kuhusu asilimia 23 linahusu wale ambao ni Watumishi wa Umma ambao wako kwenye mishahara, kwa hiyo, kwa madiwani bado wako katika sehemu ya posho, ndiyo maana tumesema tunatafuta vyanzo vingine ili kuhakikisha kwamba tunawaongezea posho Madiwani.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)