Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 29 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 252 2022-05-24

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itajenga Sport Arena katika Wilaya ya Ubungo?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, naomba kujibu swali namba 252 la Mheshimiwa Issa Jumanne Mtemvu, Mbunge Kibamba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara inaendelea na mpango wa ujenzi wa Sports and Arts Arena katika Mikoa ya Dar es Salaam na Dodoma yenye thamani ya jumla ya Shilingi za Kianzania bilioni 550 kwa ushirikiano wa Serikali na Wadau. Wizara imeshakamilisha hatua za awali za kutengeneza michoro ya Arena hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, vikao vya mashauriano baina ya Wizara na Mkoa wa Dar es Salaam vinaendelea ili kukubaliana sehemu ya ujenzi wa viwanja hivyo. Eneo la Luguruni lililopo Manispaa ya Ubungo lenye ukubwa wa ekari 10.5 ni kati ya maeneo yanayotarajiwa kupendekezwa kwa ujenzi wa mradi huo. Baada ya kukamilika kwa hatua hizo, ujenzi utaanza mara moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha. (Makofi)