Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Sport Arena katika Wilaya ya Ubungo?

Supplementary Question 1

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri sana na yenye matumaini kwa wananchi wa Wilaya ya Ubungo;:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa vikao vya mashauriano baina ya Wizara na Mkoa wa Dar es Salaam vinaendelea kuona uwezekano wa kujenga hiyo Sport Arena katika eneo la Luguruni la ekari 10.5 lililotolewa na Mheshimiwa Rais:-

(a) Je, Serikali au wizara mpo tayari sasa kumshirikisha Mheshimiwa Mbunge katika vikao hivyo kama mdau?

(b) Pamoja na nia nzuri ya Serikali ya kujenga Arena hiyo, ikiwa sasa tayari imeshakamilisha ile michoro yote ya Arena: Je, Serikali imeweza kuzingatia au kuweka miundombinu ya kuingia na kutoka katika Arena hizo?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mtemvu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi Wizara hatuna tatizo kushirikisha Wabunge. Hivyo niagize BMT na Mkurugenzi wetu wa Michezo, watakapokutana na Uongozi wa Dar es Salaam, wawashirikishe Wabunge wote wa Mkoa wa Dar es Salaam. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili alitaka kufahamu kama hiyo michoro imezingatia miundombinu mbalimbali ya kuingilia na kutokea katika viwanja hivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumezingatia hili. (Makofi)

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Sport Arena katika Wilaya ya Ubungo?

Supplementary Question 2

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza: Je, ni lini ujenzi wa shule 56 za michezo utaanza kama Serikali ambavyo iliahidi? (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo naomba kujibu swali la Mheshimiwa Asia Halamga, Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mchakato umeshaanza wa kujenga Academy 56 katika shule zetu za Sekondari na tunatarajia katika mwaka huu wa fedha ambao tunauendea, endapo Bunge lako Tukufu litatupitishia fedha, tumetenga kiasi cha Shilingi bilioni mbili kwa kuanza na shule hizo.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Sport Arena katika Wilaya ya Ubungo?

Supplementary Question 3

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kama ilivyo changamoto wenzangu walivyosema, sisi ma-promoter wa ngumi, wachezaji wetu wa ngumi hawana maeneo ya kufanyia mazoezi. Ni lini Serikali itajenga maeneo ya mazoezi ya mabondia wote hapa nchini Tanzania? (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sophia Mwakagenda, Bondia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika viwanja hivi ambavyo nimesema tunategemea kujenga Dar es Salaam na Dodoma ambavyo viko katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi; hivi viwanja vimezingatia michezo yote, in door games pia zimezingatiwa pamoja na ngumi. (Makofi)

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Sport Arena katika Wilaya ya Ubungo?

Supplementary Question 4

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Mheshimiwa Naibu Waziri ni takribani mwaka mmoja umeisha tangu Rais atoe maelekezo kwenye Wizara kufanya marekebisho ya viwanja nchini, lakini hadi sasa hakuna kiwanja kilichofanyiwa marekebisho kupitia Wizara:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni ipi kauli ya Serikali kwa sababu hali ya viwanja nchini ni mbaya na bado wanamichezo wanazidi kuweka matumaini kwa Serikali?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sanga, Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi Wizara tunashirikiana na wadau mbalimbali kurekebisha viwanja. Hivi ninavyoongea, sasa hivi tunakamilisha maridhiano na Chama cha Mapinduzi ambao wanamiliki viwanja nchi nzima kwenye mikoa, vile viwanja vikubwa, na tunategemea tutaanza ukarabati wa viwanja hivi na mwaka huu unaoanza Mheshimiwa Sanga tutaanza na viwanja saba. Tumetenga zaidi ya Shilingi bilioni 10 kwa ajili ya ukarabati wa hivi viwanja. (Makofi)