Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 29 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 254 2022-05-24

Name

Agnesta Lambert Kaiza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE K.n.y. MHE. AGNESTA L. KAIZA auliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati Magereza ili kulinda haki za wafungwa na mahabusu?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Agnesta Lambert Kaiza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Jeshi la Magereza limejipanga kukarabati Magereza kwa kutumia fedha za vyanzo vya ndani na fedha inayotengwa kwenye bajeti kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Katika mwaka 2021/2022 Serikali ilitenga Shilingi 840,000,000/= kwa ajili ya ukarabati wa Magereza matano ambayo ni Gereza Maweni, Isanga, Kondoa, Lindi na Mkuza na limetumia vyanzo vya ndani kukarabati Magereza yafuatayo: Gereza Rombo, Ukonga, Mkono wa Mara, Kwitanga, Idete, Mbigili, Shinyanga, King’ang’a, Butimba, Luanda, Liwale na Babati.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka wa fedha 2022/2023 Jeshi la Magereza limetenga Shilingi 4,569,000,000/= ili kujenga Magereza sita ya Wilaya za Kilosa, Kaliua, Karatu, Kakonko, Gairo na Msalato.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. (Makofi)