Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE K.n.y. MHE. AGNESTA L. KAIZA auliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati Magereza ili kulinda haki za wafungwa na mahabusu?

Supplementary Question 1

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu hayo wafungwa na mahabusu wamekuwa wakifanyiwa ukaguzi hadharani kwa kuvua nguo zote bila kujali umri wao; na kwa uzoefu wangu mimi, upo uwezekano wa kuwakagua kwa kuwatenganisha lakini kuweka chumba maalum, lakini Serikali imekuwa haifanyi hivyo; pamoja na kwamba Serikali imenunua scanner 12 kwa ajili ya kufanya ukaguzi: Ni kwa nini sasa Serikali isione haja ya kutenga chumba maalum kwa ajili ya kuwakagua na kuwatenganisha ili kulinda staha na haki za binadamu? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili: mavazi ya wafungwa yamechakaa mno jambo ambalo linasababisha wafungwa wanawake warithi mpaka nguo za ndani za wafungwa wenzao ambao walimaliza muda wao, jambo ambalo kwa kweli siyo sawa: Ni kwa nini sasa Serikali isione haja kwanza ya kuondoa utaratibu huo na pia kupeleka mavazi kwa ajili ya wafungwa, pamoja na magodoro, mablanketi na neti?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Nusrat Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Mbunge lakini swali letu la msingi lilikuwa linazungumzia kukarabati magereza sasa imeibuka hili la mavazi na kukaguliwa hadharani. Lakini nadhani tupokee katika ukarabati na ujenzi wa magereza yanayokuja tutazingatia umuhimu wa kuwatenganisha wafungwa wote wanaume na wanawake wakati ukaguzi unapofanyika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu mavazi kuchakaa kama mlivyosikia wakati wa bajeti, bajeti yetu mwaka huu imeongezeka kiasi ambacho maeneo ambayo yalikuwa hayapati funding kama haya ya mavazi ya wafungwa yatapewa kipaumbele ili waweze kupata mavazi yanayowastiri nakuleta staha kwa jumuiya hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE K.n.y. MHE. AGNESTA L. KAIZA auliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati Magereza ili kulinda haki za wafungwa na mahabusu?

Supplementary Question 2

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Magari yanayotumika kuwapeleka mahabusu na wafungwa mahakamani kwenda na kurudi yana uchakavu mkubwa sana. Ni lini sasa Serikali itafanya utaratibu wa kubadilisha magari hayo?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deo Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwamba ni kweli kwamba magari katika maeneo mengi yamechakaa na kama mtakumbuka tumesema mwaka huu kuna bajeti imeongezeka haitaweza kutatua matatizo yote ya uchakavu wa magari ya mahabusu lakini at least tutaanza kununua kulingana na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE K.n.y. MHE. AGNESTA L. KAIZA auliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati Magereza ili kulinda haki za wafungwa na mahabusu?

Supplementary Question 3

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Gereza la Mbulu lilijengwa toka ukoloni, na kwa kuwa gereza hilo haliko kwenye magereza yaliyotajwa hivi sasa kwenye mpango wa ujenzi. Je, ni lini Serikali itajenga upya gereza la Mbulu na makazi ya Askari?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyokwisha kusema katika jibu la msingi kulingana na upatikanaji wa fedha tutaendelea kukarabati magereza yote yaliyochoka ikiwemo hili gereza la Mbulu. Lakini kwa mwaka huu wa fedha tumebainisha magereza yaliyotengwa kwa sababu ya ndio fedha tuliyopata lakini kwa miaka ijayo gereza lake pia litafikiriwa.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE K.n.y. MHE. AGNESTA L. KAIZA auliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati Magereza ili kulinda haki za wafungwa na mahabusu?

Supplementary Question 4

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, Gereza la Tarime limejengwa tangu mwaka 1942. Miundombinu imechakaa ya maji safi na maji taka. Na kwa kuwa wakati Naibu Waziri anajibu hapa amesema hawategemei vyanzo vya ndani na Gereza la Tarime hatuna vyanzo vya ndani. Ningependa kujua mango Madhubuti wa Serikali wa kuhakikisha kwamba wanakarabati miundombinu ya maji safi na taka ili wale watu waweze huduma hii bila matatizo?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Matiko Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba magereza mengi likiwemo hili Gereza la Tarime limejengwa siku nyingi na ni moja ya magereza yaliyochakaa. Kama nilivyokwishasema katika jibu letu la msingi kulingana na upatikanaji wa fedha gereza hili pia litapewa kipaumbele angalau katika bajeti za miaka miwili ijayo, ahhsante sana.