Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 29 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 255 2022-05-24

Name

Tecla Mohamedi Ungele

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha miundombinu ya Gereza la Liwale?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tecla Mohamed Ungele Mbunge wa Viti Maalum Lindi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Jeshi la Magereza imeanza kuboresha miundombinu ya Gereza Liwale kwa kutumia fedha za vyanzo vya ndani. Jeshi la Magereza limejenga jengo jipya la Utawala na nyumba saba za watumishi kwa ajili ya kuishi askari. Majengo hayo yamekamilika na yamezinduliwa na Mwenge wa Uhuru tarehe 29 Aprili, 2022. Ili kukamilisha uboreshaji wa miundombinu iliyobakia, Shilingi 225,000,000.00 zimetengwa katika bajeti ya mwaka 2022/2023. Aidha, nawashukuru na kuwapongeza Mhe. Mbunge wa Jimbo la Liwale, Mheshimiwa Kuchauka, na Mkuu wa Wilaya ya Liwale kwa kuchangia mifuko ya saruji iliyosaidia ujenzi wa majengo ya utawala na selo moja ya Wanawake.