Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tecla Mohamedi Ungele

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha miundombinu ya Gereza la Liwale?

Supplementary Question 1

MHE. TECLA M. UNGELE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Serikali, nina swali la nyongeza. Kwa kuwa uzio ni muhimu katika mazingira ya magereza. Je, nini kauli ya Serikali kujenga uzio ulioko imara kwa Gereza la Liwale na Nachingea kwa sababu kwa sasa iko kwa kiasi cha miti imejengwa kwa miti? Ahsante.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Tecla Mohamed Ungele Mbunge wa Viti Maalum Lindi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama alivyokwishasema uzio ni kitu muhimu katika magereza yetu na kwa vile ukarabati unaendelea nitumie nafasi hii kumtaka Mkuu wa Gereza la Liwale aendelee katika mipango yake kuweka kipaumbele katika uzio ili anapomaliza ukarabati wa majengo hayo basi uzio pia uweze kuendelezwa.

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha miundombinu ya Gereza la Liwale?

Supplementary Question 2

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kuna Gereza la Ngwala ambalo liko Wilaya ya Songwe, Mkoani Songwe, ambalo ni gereza kongwe na kwa sasa limechakaa sana. Nilifanya ziara pale nikagundua kwamba idadi ya askari walioko pale ni wengi kuliko maelezo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni nini mkakati wa Wizara kuhakikisha Gereza lile kwanza linapokea wafungwa wengi na kukarabatiwa? Ahsante.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Neema kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyokwishasema kwenye jibu la msingi ni kipaumbele cha Serikali kukarabati magereza yote yaliyochoka kulingana na upatikanaji wa fedha. Kwa kuwa mwaka huu gereza hili halimo hili la Mkoa wa Songwe basi tutalipa kipaumbele katika ukarabati katika miaka ijayo ya bajeti, nashukuru.