Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 29 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 256 2022-05-24

Name

Michael Mwita Kembaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Mjini

Primary Question

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka umeme kwenye mitaa 61 katika Mji wa Tarime?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Michael Mwita Kembaki, Mbunge wa Tarime Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mamlaka ya Mji wa Tarime ina jumla ya mitaa 81. Kati ya Mitaa hiyo, Mitaa 53 ina umeme na Mitaa 28 haijapata huduma ya umeme. Mitaa minne ya Nyamiobo, Kogesenda, Itununu, na Nguku itapatiwa huduma ya umeme kupitia Mradi wa ujazilizi (Densification 2C) unaotarajiwa kuanza mwezi Agosti, 2022. Mitaa mingine 24 iliyobaki inaendelea kupatiwa huduma ya umeme na TANESCO kadri ya upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea na jitihada za kutafuta fedha kwa ajili ya kufikisha umeme katika mitaa yote katika kipindi kifupi kijacho.