Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Michael Mwita Kembaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Mjini

Primary Question

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka umeme kwenye mitaa 61 katika Mji wa Tarime?

Supplementary Question 1

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nina maswali mawili ya nyongeza. Lakini Shirika letu la Umeme TANESCO Ta rime linafanya kazi nzuri ya kusambaza umeme ingawa wanafanya kwa mazingira magumu hawana gari. Ningeomba Serikali wawapatie gari ili warahisishe usambazaji wa umeme katika Mji wetu wa Tarime.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kumekuwepo na utamaduni wa kurundika nguzo katika mitaa na nguzo hizo zinakaa muda mrefu kwa mfano katika Mtaa wa Ugete kuna nguzo zimekaa pale miaka miwili sasa na mpaka sasa hazijasambazwa. Je, ni lini nguzo hizi zitasambazwa ili wananchi waweze kupata umeme? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kumekuwepo na utamaduni wa kupeleka umeme katika kaya moja katika mtaa. Kwa hivyo kaya nyingi katika mitaa hiyo inayofata haina umeme. Ni lini Serikali itasambaza umeme katika kaya hizi ambazo hazijapata umeme katika mitaa hiyo? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Michael Kembaki Mbunge wa Tarime Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nikubali kwamba, miundombinu na vitendea kazi tulivyokuwa navyo havitoshi lakini Serikali inaendelea kujihimu na katika bajeti inayokuja tunataraji kupata magari na vitendea kazi vingine na kuvisambaza katika maeneo yenye uhitaji kwa ajili ya kuweza kuwezesha utendaji wa kazi nzuri. Naamini na Tarime Mjini pia itanufaika na matengenezo na mafanikio hayo ambayo tutakuwa tumeyapata.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye maswali mawili ya nyongeza nimwakikishie Mheshimiwa Kembaki kwamba katika bajeti inayokuja tumetengewa fedha za kutosha na Mheshimiwa Rais ametuhakikishia kuzipata kwa ajili ya kukamilisha hiyo miradi ambayo imekuwa ni viporo kama inaonekana nguzo zimelala miradi haijakamilika lakini na kuongeza wigo wa kupeleka umeme katika maeneo yetu kuanzia kwenye maeneo ya vijiji pia kwenye maeneo ya mitaa. Kwa hiyo, tutakuwa na nafasi nzuri ya kupanua wigo wa kupeleka umeme kwenye maeneo mbalimbali kuanzia mwaka ujao wa fedha kwa sababu tunatarajia kupata fedha nyingi zaidi.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka umeme kwenye mitaa 61 katika Mji wa Tarime?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Ni lini Serikali itasambaza umeme katika vijiji 202 vya Mkoa wa Simiyu vilivyobaki ili viweze kupatiwa umeme?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Midimu Mbunge wa Mkoa wa Simiyu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwamba tayari REA III Round II inaendelea katika maeneo yote ya Tanzania katika maeneo ya vijiji ambavyo havikuwa na umeme na tunaamini kufikia Desemba tutakuwa tumekamilisha kwenye baadhi ya maeneo na wengine wataendelea kukamilisha kwa mujibu wa ratiba walizokuwanazo. Kwa hiyo, umeme katika eneo lake utaendelea kupelekwa na kuwafikia wananchi.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka umeme kwenye mitaa 61 katika Mji wa Tarime?

Supplementary Question 3

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi, tatizo lililoko Tarime Mjini ni sawasawa na tatizo lililoko kwenye Halmashauri ya Msalala. Kwa kuwa Serikali imekuwa ikitumia fedha nyingi kupeleka umeme kwenye makao makuu ya vijiji na hivyo kupelekea baadhi ya mitaa kukosa huduma ya umeme. Ni lini Serikali itaanza umeme kwenye mitaa ya Kata ya Bulyamuru, Segese, Isaka na Burige?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Iddi Kassim Iddi Mbunge wa Msalala kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama tulivyosema kwenye jibu la msingi mitaa yote ambayo haijafikiwa na umeme katika mwaka wa fedha unaokuja, tunayo program yetu ya Densification 2B na 2C itahakikisha inafikisha umeme katika maeneo hayo kwa kadri ya upatikanaji wa fedha.

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka umeme kwenye mitaa 61 katika Mji wa Tarime?

Supplementary Question 4

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi, naomba kuuliza Mkandarasi wa Mbogwe aliripoti toka mwaka jana lakini mpaka sasa hivi hakuna kazi inayofanyika, vijiji 34 havijapatiwa umeme. Ni nini kauli ya Serikali?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maganga Mbunge wa Mbogwe kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi ya REA III Round II inaendelea katika hatua mbalimbali katika maeneo yetu, kama ambavyo tumewahi kueleza hapa Bungeni kwamba miradi ya REA III round II inazo hatua kadhaa za kufikia ili kuweza mradi kukamilika katika utekelezaji wake. Kwa hiyo, nimwakikishie Mheshimiwa Maganga kwamba naamini katika eneo lake hatua mojawapo katika mradi huo itakuwa inaendelea. Lakini nimwombe kwa sababu lipo banda letu hap ana mkandarasi anayetengeneza mradi huo yuko hapa, Meneja wa Wilaya yuko hapa, Meneja wa Mkoa yuko hapa basi tutembelee pale na tuweze kujua tatizo na kero ambazo zipo.

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka umeme kwenye mitaa 61 katika Mji wa Tarime?

Supplementary Question 5

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Mheshimiwa Waziri Kata ya Lahoda, Sanzawa- Mpendo na Kinyamshindo zilikuwa zipate umeme REA phase II lakini hazikufanyiwa hivyo. Na sasa tuko kipindi cha REA phase III. Nini mkakati wa Serikali wa kuhakikisha kata hizi na vijiji vyake vinapata umeme katika Mradi huu wa REA phase III? ahsante.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kunti Majala kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya REA III round II kuisha ninatoa maelezo ya Serikali hakuna Kijiji kitakuwa hakijafikiwa na Nishati ya Umeme. Commitment ya Serikali ni kuhakikisha kwamba katika awamu hii ya tatu mzunguko wa pili vijiji vyote Tanzania Bara vinapata umeme. Kwa hiyo, nimwakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba eneo hilo pia litapata umeme.