Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 35 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 306 2022-06-01

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza:-

Je, ni lini ujenzi wa Vituo vya Afya Kata za Mundindi, Lupingu, Lupanga, Ludende, Madilu, Ludewa, Lugarawa na Mawengi utakamilika?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Zacharius Kamonga, Mbunge wa Jimbo la Ludewa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali katika mwaka wa fedha 2021/2022 imekwishapeleka Shilingi Milioni 500 kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa kwa ajili ya ukamilishaji wa Kituo cha Afya Mundindi kilichopo katika Kata ya Mundindi. Ujenzi wa jengo la la wagonjwa wa nje (OPD) na maabara umekwishakamilika na majengo mengine yapo kwenye hatua mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeainisha maeneo ya kimkakati ya kujenga vituo vya afya katika Wilaya ya Ludewa kwa awamu kadri ya bajeti ya Serikali. Ahsante.