Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa Vituo vya Afya Kata za Mundindi, Lupingu, Lupanga, Ludende, Madilu, Ludewa, Lugarawa na Mawengi utakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Naomba kufahamu ni lini Serikali itatujengea Kituo cha Afya, katika Kata ya Bara ili kupunguza idadi ya vifo vya mama na mtoto katika Wilaya ya Mbozi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Juliana Shonza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeandaa mkakati, kwanza wa kukamilisha vituo vyote zahanati na hospitali za Halmashauri ambazo zimekamilika lakini hazijaanza kutoa huduma. Baada ya hapo tutakwenda sasa kujenga vituo vya afya kwenye maeneo ya kimkakati likiwemo eneo hili ambalo Mheshimiwa Juliana Shonza amelisema.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimhakikishie kwamba tutakwenda kuhakikisha kwamba tunajenga pia kituo cha afya baada ya kukamilisha vituo vingine.

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa Vituo vya Afya Kata za Mundindi, Lupingu, Lupanga, Ludende, Madilu, Ludewa, Lugarawa na Mawengi utakamilika?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali, pamoja na hivyo naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kwa kuwa wananchi wa Ludewa wamevuja jasho sana kuanza ujenzi kwenye Kata 12, Je, ni lini Mheshimiwa Waziri yuko tayari kuambatana na mimi ili kwenda kushuhudia jinsi wananchi walivyojitoa kutoa kujenga vituo vya afya na havijamaliziwa na Serikali?

Swali la pili, kwa kuwa Tarafa ya Mwambao haina usafiri wa magari na meli kwa muda mrefu haipo. Je, ni kwanini Serikali isitafute boti moja ya mwendokasi ambayo itasaidia wagonjwa kuanzia Lumbila, Kilondo, Makonde, Lifuma, Mkali mpaka Manda?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Joseph Zacharius Kamonga, Mbunge wa Jimbo la Ludewa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Kamonga, amekuwa akifuatilia sana miradi ya maendeleo kwa ajili ya wananchi wa Jimbo la Ludewa, ikiwemo vituo vya afya na magari ya magonjwa. Kwa kweli katika Kata hizi 12 ambazo wananchi wamechangia nguvu zao kujenga vituo vya afya, nimhakikishie kwamba Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuunga mkono juhudi za wananchi kukamilisha vituo hivi.

Mheshimiwa Spika, nitoe maelekezo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa, kwa mwaka ujao wa fedha baada ya mwaka huu ambao tumeshaupangia bajeti atenge fedha kwa ajili ya kujenga maabara na kichomea taka kwenye vituo ambavyo wananchi wameshaweka nguvu zao, ili huduma za OPD zianze na Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya kukamilisha vituo hivyo.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na ambulance, boti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunafanya tathmini maeneo yote ambayo ni magumu kufikika ya visiwa na ambayo yanapitiwa na mikondo ya maji, tuangalie uwezekano wa kupata ambulance hizi za boti kwa kadri ya upatikanaji wa fedha na tutatoa kipaumbele kwenye Wilaya ya Ludewa.

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa Vituo vya Afya Kata za Mundindi, Lupingu, Lupanga, Ludende, Madilu, Ludewa, Lugarawa na Mawengi utakamilika?

Supplementary Question 3

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Afya katika Kata ya Miula Jimbo la Nkasi Kusini?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imeshaweka mkakati wa kuainisha maeneo ya kujenga vituo vya afya, ikiwemo katika Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi, kwa hivyo, kadri ya upatikanaji wa fedha katika bajeti inayofuata tutahakikisha tunatenga fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa vituo vya afya katika maeneo hayo. Ahsante.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa Vituo vya Afya Kata za Mundindi, Lupingu, Lupanga, Ludende, Madilu, Ludewa, Lugarawa na Mawengi utakamilika?

Supplementary Question 4

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Jimbo la Tabora Mjini lenye Kata 29 kuna Kata ya Tumbi pamoja na Kata ya Misha tayari vituo vya afya vimeashaanza kujengwa na vipo katika hali ile ya kumalizia. Ni lini Serikali italeta fedha hizi za kumalizia vituo hivyo vya afya viwili?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Emmanuel Mwakasaka, Mbunge wa Jimbo la Tabora Mjini kama ifutavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunatambua kwamba kata nyingi bado zinahitaji vituo vya afya, lakini Kata za mkakati tumekwishaziainisha na Waheshimiwa Wabunge, walileta Kata za kipaumbele tatu kila Jimbo, niwahakikishie kwamba Serikali inaendelea kuandaa bajeti kwa ajili ya kuendelea na ukamilishaji wa vituo hivi vya afya, vikiwemo hivi vituo vya afya viwili ambavyo vipo katika Jimbo la Tabora Mjini.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa Vituo vya Afya Kata za Mundindi, Lupingu, Lupanga, Ludende, Madilu, Ludewa, Lugarawa na Mawengi utakamilika?

Supplementary Question 5

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Serikali ndiyo ilihamasisha ujenzi wa vituo vya afya katika maeneo mbalimbali nchi nzima na kuwahamasisha wananchi washiriki lakini leo hazijakamilisha. Je, mliamua kuwahamasisha wananchi bila kuwa na fedha za kutosha ndiyo maana kila Mbunge leo anaulizia kituo cha afya. Kwa nini sasa msikamilishe wakati ninyi ndiyo mliwahamasisha wananchi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ester Bulaya, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza tukubaliane kwamba kuhamasisha wananchi kuchangia nguvu zao katika ujenzi wa vituo vya afya ni dhamira njema na jambo jema kwa sababu wananchi wetu wamekuwa wanasafiri umbali mrefu sana kupata huduma za afya. Kwa hiyo, kwa kuanza tu jambo hilo lilikuwa ni jema na nia njema ya Serikali lakini tumeendelea kutenga fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma.

Mheshimiwa Spika, mwaka uliopita maboma 555 ya zahanati Bilioni 33.5 zilipelekwa, mwaka huu tumepeleka katika maboma zaidi ya 234 ya vituo vya afya na zahanati. Mwaka ujao tunayo maboma 300 ya zahanati ambayo yanakwenda kukamilishwa. Kwa hiyo, Serikali inafanya kazi ya kukamilisha maboma hayo kwa nia njema ya kusogeza huduma kwa wananchi, lakini safari ni hatua, tutakwenda kwa awamu mpaka kukamilisha majengo hayo yote. (Makofi)